HADITHI: SAFARI YA KWANZA KUZIMU 3
MWANDISHI: NYEMO CHILONGANI
MWANDISHI: NYEMO CHILONGANI
Nilikuwa nikijifikiria kuhusu huyo mkuu wa makaburuni aliyetarajiwa kufika mahali hapo, sikujua alikuwa vipi na alifanana vipi. Wachawi wale waliokuwa makaburini pale waliendelea kula nyama za watu.
Zilipita kama dakika mbili hivi, ghafla wachawi wale waliokuwa wakizungumza yao huku wakisherehekea kwa kula nyama zile nikawaona wakikaa kimya na kiviinamisha vichwa vyao chini kama ishara ya kutoa heshima fulani.
Hapohapo nikaanza kusikia tena baridi kama nililolisikia kipindi cha nyuma. Kwa wakati huu, baridi lile liliambatana na upepo mkali huku nikisikia majani ya miti yakilia vuuu vuuu muda wote.
Mara nikaanza kusikia milio mikubwa kama ngurumo za radi makaburini pale huku kwa mbali kukiwa kama na tetemeko la ardhi. Kiukweli niliogopa lakini nikajua ndiyo kwanza yule mkuu wa makaburini alikuwa akifika mahali hapo, nilichokifanya ni kusubiri ili na mimi nimuone.
Kwa mbali nikaanza kumuona mtu mkubwa sana akija, alionekana kuwa na mwili mkubwa kama walivyo wacheza mpira wa kikapu wa Marekani. Alikuwa amejazajaza. Alipokuwa kwa mbali nilimuona kuwa binadamu wa kawaida kwa sababu ya giza lakini mara aliposogea kule walipokuwa wale wachawi ndipo nikagundua kwamba hakuwa binadamu wa kawaida.
Mwili wake ulikuwa na manyoya mengi kama simba, miguu ilifanana na miguu ya sokwe, hakuwa na uso wa binadamu, alikuwa na uso wa mbweha huku kichwani akiwa na mapembe makubwa mithiri ya urefu wa chupa ya soda na masikio makubwa mithiri ya sahani ya chakula.
Jitu lile la ajabu lilipokuwa likitembea, bado wachawi walikuwa wameviinamisha vichwa vyao chini kama kumpa heshima yake, lilitembea mpaka mbele kabisa, juu ya kaburi moja ambalo kwa juu kulikuwa na sinia jingine lililokuwa na nyama na jagi lenye damu za watu kisha kuanza kula.
Hakuwa akitafuna kama binadamu wa kawaida wanapotafuta vitu bali alikuwa akitafuna kana kwamba alitafuta kitu kigumu tena alichotakiwa kukimaliza kwa haraka sana.
Nilishindwa kuvumilia kubaki mahali hapo kwani kila nilipokuwa nikiliangalia lile jitu la kutisha, mwili wangu ulikuwa ukisisimka tu, nilichokifanya ni kumwambia Yusnath kwamba ninataka kuondoka.
“Umeridhika?” aliniuliza.
“Ndiyo! Naomba tuondoke,” nilimwambia.
Akaunyoosha mkono wake, ghafla pale nilipokuwa nikaanza kuvutwa lakini sikukiona kile kilichokuwa kikinivuta. Nilipelekwa mpaka kule alipokuwa Yusnath na aliponishika mkono tu, tukapotea na kuibukia kule mlimani.
Pale mlimani hatukukaa sana, akaniambia niyafumbe macho yangu kwani sehemu tuliyokuwa tukienda ilikuwa na watu wengi lakini hiyo njia ambayo tulitakiwa kuipita ilikuwa na mauzauza mengi ambayo hakutaka niyaone. Hilo halikuwa tatizo, nikayafumba macho yangu.
Ghafla tukaibukia sehemu ambayo ilikuwa na watu wengi mbele yetu, watu wale walikuwa wameviinamisha vichwa vyao, walikuwa wengi zaidi ya watu elfu moja. Nikaanza kujiuliza watu wale walikuwa mahali pale wanafanya nini.
“Hawa ni wenzako kutoka duniani ambao wamefika hapa kwa ajili ya kumuabudu mkuu wetu,” alinijibu Yusnath japokuwa swali lile nilijiuliza moyoni mwangu na sikujua alijuaje kama nilijiuliza vile.
“Kuna ninaowafahamu?”
“Wapo wengi tu, unataka kuwaona?”
“Ndiyo!”
“Basi subiri!”
Niliendelea kusubiri, nikawa na kiu kubwa ya kutaka kuwaona hao watu waliokuwa mahali hapo ambapo Yusnath aliniambia kwamba kulikuwa na wengine niliokuwa nikiwafahamu kabisa.
Nilisubiri mpaka baada ya dakika kadhaa, nikasikia muungurumo mkubwa mithiri ya simba, Yusnath akaniambia nifumbe macho kwani yule aliyekuwa akija ndiye alikuwa kiongozi wao, yaani shetani mkuu.
Kwanza nikajifanya kupinga kimoyomoyo kwani nilihisi kutokana na mahali hapo kuwa usiku basi Yusnath asingeweza kuona kama macho yangu hayakufumbwa bali nilikuwa naangalia kisirisiri tu.
Muungurumo ule uliendelea kusikika na mara kule ambapo Yusnath aliponaimbia kwamba ndiyo ingekuwa njia ya shetani kufika mahali hapo kukaanza kufuka moshi mkubwa na mzito, tena ulikuwa ukifuka kwa kasi kubwa.
Nilibaki nikiangalia tu, ghafla nikaanza kuyaona macho yangu yakiwa mazito. Nilijitahidi sana kuyaacha wazi lakini ikashindikana, nikashtukia yakiwa yamefumba kabisa kitu kilichonifanya nikubaliane nacho.
Nikasikia kishindo kikubwa cha mtu aliyekuwa akitembea, kishindo kile hakikuwa cha kawaida hata kidogo na alikuwa akitembea kuelekea kule kulipokuwa na watu wengi waliokuwa wameinamisha vichwa kama ishara ya kumuabudu.
Sikujua alikuwa akifanya nini, ila baada ya dakika kama kumi, nikaambiwa niyafumbue macho yangu, nikafanya hivyo. Yule shetani hakuwepo tena, alikuwa amekwishaondoka na nilipowaangalia wale watu ambao waliyainua macho yao, sikuamini kabisa kama watu kama hao ningeweza kuwakuta mahali hapo.
Mtu wa kwanza kabisa kumuona, aliitwa Fabian Joseph. Huyu alikuwa mchungaji wa kanisa fulani hivi lililokuwa maarufu sana huku duniani nchini Tanzania. Waumini wengi walikwenda kwake kuabudu, aliponya wagonjwa kwa kuwapaka mafuta ambayo kwake alisema kwamba aliyatoa Israel.
Viwete walitembea, hakufanya hivyo tu bali kulikuwa na miujiza mingi aliyokuwa akitokea kanisani kwake. Leo hii, mchungaji huyo ambaye alijiita mtume, naye alikuwepo huko kuzimu akipewa nguvu.
Hebu ngoja nikwambie vizuri kuhusu huyu mchungaji.
*****
Kanisa lilianza kama utani, nakumbuka kipindi kile kulikuwa na washirika kama wanne, watu wengi waliokuwa wakipita karibu na kanisa lile, walikuwa wakishangaa ilikuwaje mchungaji awe na nguvu ya kutoa huduma na wakati watu walikuwa wachache sana.
Watu tulipuuzia, mchungaji yule ambaye alipenda sana kujiita mtume akaanza kuchapisha matangazo na kuyabandika mitaani kwamba alikuwa akiponya magonjwa mbalimbali, wanawake waliokuwa tasa waliitwa pia kwa ajili ya kuwekewa mikono na kupokea uponyaji.
Hilo halikuwafanya watu kulisogelea kanisa lile kwani kitu walichokuwa wakikihitaji ni kuona miujiza ili waamini. Baada ya mwezi mmoja, watu walewale wanne waliokuwa ndani ya kanisa lile wakaanza kuwaambia watu wengine kwamba kulikuwa na miujiza ilikuwa ikitendeka hivyo watu wawapeleke wagonjwa kwa mtume yule.
Kama unavyojua binadamu kuna kitu kujaribu. Kuna mwanamke aliyekuwa akiishi karibu na mtaa uliokuwa na kanisa lile, miaka nenda rudi alikuwa na kibiongo. Watu walimuonea huruma sana lakini baada ya kusikia kile kilichozungumziwa kuhusu mtume na miujiza aliyotarajiwa kuitoa, mwanamke yule akaingia.
Sijui nini kilitokea kanisani lakini siku moja baadae nilipomuona mwanamke yule, hakuwa na kibiongo. Hapo ndipo watu walipoanza kuamini kwamba ile miujiza iliyokuwa ikitangazwa kweli ilikuwa ikifanyika, kanisa likaanza kujaza watu.
“Nilifahamu hilo tu, hebu niambie kingine nisichokijua,” nilimwambia Yusnath.
“Subiri,” aliniambia na kunipeleka sehemu iliyokuwa na kitu kikubwa kama televisheni na kuanza kunionyeshea maisha halisi ya mchungaji yule.
Lile kanisa halikuwa kanisa kama tulivyokuwa tukiliona, lilikuwa pango kubwa ambalo lilikuwa na muonekanao wa kichwa cha paka, mlangoni kulikuwa na miti mikubwa iliyokuwa imesimikwa huku juu yake kukiwa na mafuvu mawili ya binadamu na mafuvu mengine ya mnyama nisiyemfahamu.
Mlangoni hapo kulikuwa na mtungi mkubwa wa damu, kila mshirika aliyekuwa akiingia kanisa, ilikuwa ni lazima kuinama mlangoni kisha kuingia. Unapoinama pale mlangoni, unauinamia ule mtungi bila kujua na katika hali ambayo sikuifahamu, kuna kiasi kidogo cha damu unachangia katika mtungi ule.
Unajiona kwamba umevaa nguo lakini unapouvuka mlango wa kuingia kanisani, nguo zako zinaachwa mlangoni na wewe kuingia mtupu.
Kanisani mule hakukuwa na washirika tu bali kulikuwa na viumbe vingine vya ajabu ambavyo kazi zao zilikuwa zilezile za kuwavuta watu. Viumbe hivyo vya ajabu havikuwa ndani ya kanisa tu bali vilikuwepo mpaka pale nje.
Ushawahi kupita nje ya kanisa fulani, unasikia kuwa na hamu ya ghafla kuingia kanisani humo kwa ajili ya kuabudu? Yaani moyo wako unakusisimka na kutamani zaidi uingie. Ndugu yangu, hiyo inakuwa ni kazi ya hivyo viumbe vya ajabu ambavyo husimama nje na kukuvuta wewe.
Nilimuona mchungaji yule akiwaombea watu, mkononi alikuwa na kitambaa cheupe, kazi yake kubwa ilikuwa ni kuwapiga watu na kile kitambaa ambacho Yusnath aliniambia kwamba kilikuwa chao na walimpa kwa ajili ya kufanyia kazi hiyo.
Mtu anapopigwa na kitambaa kile, kwanza akili yake inachanganyikiwa, hakuna kitu kingine anachokipenda zaidi ya kuingia kanisani humo na huwa mtumwa wa moja kwa moja.
Mambo niliyokuwa nikiyaona ndani ya kanisa lile yalinishtua sana. Pembeni ya kiti cha mchungaji kulikuwa na joka kubwa, kazi yake ilikuwa ni kukaa hapohapo huku akiwaangalia washirika.
Ukiachana na joka lile, kulikuwa na joka jingine ambalo lilikuwa likitembea huku na kule, kazi yake kubwa ilikuwa ni kuwatemea watu mate ambayo Yusnath aliniambia kwamba mara unapotemewa mate yale, hata kama kuna mtu atakuja na kukwambia yule mchungaji ni mchawi, mzinzi, huwezi kuamini na unaweza kugombana na mtoa taarifa.
“Kumbeeee....” nilisema.
“Kumbe nini?”
“Nilipokuwa nikipita nje ya kanisa lake nilitamani kuingia,” nilimwambia.
“Hiyo ndiyo kazi ya vile viumbe, kuwavuta nyie tu.”
“Sawa. Kuna kingine?”
Hakutaka kuniambia hivihivi tu, alitaka kunionyeshea kila kitu kupitia televisheni ile. Nilimuona mchungji akichukua mafuta fulani hivi, alijipaka mikononi, alipokuwa akimuona mshirika mwanamke mzuri, alikuwa akimfuata na kumpaka mafuta yale na kumwambia kwamba yalitoka kwa Mungu kumbe hakuna lolote lile.
Baada ya kupakwa mafuta yale, akili ya msichana huyo inachanganyikiwa, muda mwingi anamuwaza mchungaji na mwisho wa siku kulala naye kitanda kimoja.
Kila nilichokuwa nikikiangalia, kilinifanya nichukie, nilikuwa mkristo, lakini sikuwa mtu wa kwenda kanisani lakini yale yaliyokuwa yakifanywa kwa baadhi ya makanisa likiwepo lile la mchungaji huyu, lilinisikitisha sana.
“Unajua watu wanaponywa vipi magonjwa yao?” aliniuliza Yusnath.
“Hapana! Inakuwaje?”
“Njoo huku,” aliniambia, akanishika mkono na kuanza kuelekea katika chumba kimoja.
Kilikuwa kikitisha sana, kulikuwa na maiti nyingi zilizokuwa zimetobolewatobolewa, sikujua na nini lakini nyingine zilivarishwa sanda nyeupe kabisa zisizokuwa na doa hata kidogo.
Chumbani mule kulikuwa na milio ya ajabu, wakati mwingine ilisikika milio ya paka lakini wakati mwingine ya bundi, kila nilipoisikia, niliogopa sana. Yusnath hakutaka kujali, aliendelea kunishika mkono na kuelekea mbele zaidi huku sakafuni kukiwa na damu nyingi zilizokuwa zikinuka mno.
Tukafika sehemu moja iliyokuwa na uwanja mkubwa, sikujua kama ilikuwa makaburini au la, alichoniambia ni kwamba nisimame imara, nikatii, akaniambia kwamba kuna mambo mengine ya mtume huyo nitayaona, nikamwambia hakuna tatizo, hivyo nikaanza kusubiri huku mwili ukinisisimka mno kwani sehemu ile ilitisha sana.
Zilipita kama dakika mbili hivi, ghafla wachawi wale waliokuwa wakizungumza yao huku wakisherehekea kwa kula nyama zile nikawaona wakikaa kimya na kiviinamisha vichwa vyao chini kama ishara ya kutoa heshima fulani.
Hapohapo nikaanza kusikia tena baridi kama nililolisikia kipindi cha nyuma. Kwa wakati huu, baridi lile liliambatana na upepo mkali huku nikisikia majani ya miti yakilia vuuu vuuu muda wote.
Mara nikaanza kusikia milio mikubwa kama ngurumo za radi makaburini pale huku kwa mbali kukiwa kama na tetemeko la ardhi. Kiukweli niliogopa lakini nikajua ndiyo kwanza yule mkuu wa makaburini alikuwa akifika mahali hapo, nilichokifanya ni kusubiri ili na mimi nimuone.
Kwa mbali nikaanza kumuona mtu mkubwa sana akija, alionekana kuwa na mwili mkubwa kama walivyo wacheza mpira wa kikapu wa Marekani. Alikuwa amejazajaza. Alipokuwa kwa mbali nilimuona kuwa binadamu wa kawaida kwa sababu ya giza lakini mara aliposogea kule walipokuwa wale wachawi ndipo nikagundua kwamba hakuwa binadamu wa kawaida.
Mwili wake ulikuwa na manyoya mengi kama simba, miguu ilifanana na miguu ya sokwe, hakuwa na uso wa binadamu, alikuwa na uso wa mbweha huku kichwani akiwa na mapembe makubwa mithiri ya urefu wa chupa ya soda na masikio makubwa mithiri ya sahani ya chakula.
Jitu lile la ajabu lilipokuwa likitembea, bado wachawi walikuwa wameviinamisha vichwa vyao chini kama kumpa heshima yake, lilitembea mpaka mbele kabisa, juu ya kaburi moja ambalo kwa juu kulikuwa na sinia jingine lililokuwa na nyama na jagi lenye damu za watu kisha kuanza kula.
Hakuwa akitafuna kama binadamu wa kawaida wanapotafuta vitu bali alikuwa akitafuna kana kwamba alitafuta kitu kigumu tena alichotakiwa kukimaliza kwa haraka sana.
Nilishindwa kuvumilia kubaki mahali hapo kwani kila nilipokuwa nikiliangalia lile jitu la kutisha, mwili wangu ulikuwa ukisisimka tu, nilichokifanya ni kumwambia Yusnath kwamba ninataka kuondoka.
“Umeridhika?” aliniuliza.
“Ndiyo! Naomba tuondoke,” nilimwambia.
Akaunyoosha mkono wake, ghafla pale nilipokuwa nikaanza kuvutwa lakini sikukiona kile kilichokuwa kikinivuta. Nilipelekwa mpaka kule alipokuwa Yusnath na aliponishika mkono tu, tukapotea na kuibukia kule mlimani.
Pale mlimani hatukukaa sana, akaniambia niyafumbe macho yangu kwani sehemu tuliyokuwa tukienda ilikuwa na watu wengi lakini hiyo njia ambayo tulitakiwa kuipita ilikuwa na mauzauza mengi ambayo hakutaka niyaone. Hilo halikuwa tatizo, nikayafumba macho yangu.
Ghafla tukaibukia sehemu ambayo ilikuwa na watu wengi mbele yetu, watu wale walikuwa wameviinamisha vichwa vyao, walikuwa wengi zaidi ya watu elfu moja. Nikaanza kujiuliza watu wale walikuwa mahali pale wanafanya nini.
“Hawa ni wenzako kutoka duniani ambao wamefika hapa kwa ajili ya kumuabudu mkuu wetu,” alinijibu Yusnath japokuwa swali lile nilijiuliza moyoni mwangu na sikujua alijuaje kama nilijiuliza vile.
“Kuna ninaowafahamu?”
“Wapo wengi tu, unataka kuwaona?”
“Ndiyo!”
“Basi subiri!”
Niliendelea kusubiri, nikawa na kiu kubwa ya kutaka kuwaona hao watu waliokuwa mahali hapo ambapo Yusnath aliniambia kwamba kulikuwa na wengine niliokuwa nikiwafahamu kabisa.
Nilisubiri mpaka baada ya dakika kadhaa, nikasikia muungurumo mkubwa mithiri ya simba, Yusnath akaniambia nifumbe macho kwani yule aliyekuwa akija ndiye alikuwa kiongozi wao, yaani shetani mkuu.
Kwanza nikajifanya kupinga kimoyomoyo kwani nilihisi kutokana na mahali hapo kuwa usiku basi Yusnath asingeweza kuona kama macho yangu hayakufumbwa bali nilikuwa naangalia kisirisiri tu.
Muungurumo ule uliendelea kusikika na mara kule ambapo Yusnath aliponaimbia kwamba ndiyo ingekuwa njia ya shetani kufika mahali hapo kukaanza kufuka moshi mkubwa na mzito, tena ulikuwa ukifuka kwa kasi kubwa.
Nilibaki nikiangalia tu, ghafla nikaanza kuyaona macho yangu yakiwa mazito. Nilijitahidi sana kuyaacha wazi lakini ikashindikana, nikashtukia yakiwa yamefumba kabisa kitu kilichonifanya nikubaliane nacho.
Nikasikia kishindo kikubwa cha mtu aliyekuwa akitembea, kishindo kile hakikuwa cha kawaida hata kidogo na alikuwa akitembea kuelekea kule kulipokuwa na watu wengi waliokuwa wameinamisha vichwa kama ishara ya kumuabudu.
Sikujua alikuwa akifanya nini, ila baada ya dakika kama kumi, nikaambiwa niyafumbue macho yangu, nikafanya hivyo. Yule shetani hakuwepo tena, alikuwa amekwishaondoka na nilipowaangalia wale watu ambao waliyainua macho yao, sikuamini kabisa kama watu kama hao ningeweza kuwakuta mahali hapo.
Mtu wa kwanza kabisa kumuona, aliitwa Fabian Joseph. Huyu alikuwa mchungaji wa kanisa fulani hivi lililokuwa maarufu sana huku duniani nchini Tanzania. Waumini wengi walikwenda kwake kuabudu, aliponya wagonjwa kwa kuwapaka mafuta ambayo kwake alisema kwamba aliyatoa Israel.
Viwete walitembea, hakufanya hivyo tu bali kulikuwa na miujiza mingi aliyokuwa akitokea kanisani kwake. Leo hii, mchungaji huyo ambaye alijiita mtume, naye alikuwepo huko kuzimu akipewa nguvu.
Hebu ngoja nikwambie vizuri kuhusu huyu mchungaji.
*****
Kanisa lilianza kama utani, nakumbuka kipindi kile kulikuwa na washirika kama wanne, watu wengi waliokuwa wakipita karibu na kanisa lile, walikuwa wakishangaa ilikuwaje mchungaji awe na nguvu ya kutoa huduma na wakati watu walikuwa wachache sana.
Watu tulipuuzia, mchungaji yule ambaye alipenda sana kujiita mtume akaanza kuchapisha matangazo na kuyabandika mitaani kwamba alikuwa akiponya magonjwa mbalimbali, wanawake waliokuwa tasa waliitwa pia kwa ajili ya kuwekewa mikono na kupokea uponyaji.
Hilo halikuwafanya watu kulisogelea kanisa lile kwani kitu walichokuwa wakikihitaji ni kuona miujiza ili waamini. Baada ya mwezi mmoja, watu walewale wanne waliokuwa ndani ya kanisa lile wakaanza kuwaambia watu wengine kwamba kulikuwa na miujiza ilikuwa ikitendeka hivyo watu wawapeleke wagonjwa kwa mtume yule.
Kama unavyojua binadamu kuna kitu kujaribu. Kuna mwanamke aliyekuwa akiishi karibu na mtaa uliokuwa na kanisa lile, miaka nenda rudi alikuwa na kibiongo. Watu walimuonea huruma sana lakini baada ya kusikia kile kilichozungumziwa kuhusu mtume na miujiza aliyotarajiwa kuitoa, mwanamke yule akaingia.
Sijui nini kilitokea kanisani lakini siku moja baadae nilipomuona mwanamke yule, hakuwa na kibiongo. Hapo ndipo watu walipoanza kuamini kwamba ile miujiza iliyokuwa ikitangazwa kweli ilikuwa ikifanyika, kanisa likaanza kujaza watu.
“Nilifahamu hilo tu, hebu niambie kingine nisichokijua,” nilimwambia Yusnath.
“Subiri,” aliniambia na kunipeleka sehemu iliyokuwa na kitu kikubwa kama televisheni na kuanza kunionyeshea maisha halisi ya mchungaji yule.
Lile kanisa halikuwa kanisa kama tulivyokuwa tukiliona, lilikuwa pango kubwa ambalo lilikuwa na muonekanao wa kichwa cha paka, mlangoni kulikuwa na miti mikubwa iliyokuwa imesimikwa huku juu yake kukiwa na mafuvu mawili ya binadamu na mafuvu mengine ya mnyama nisiyemfahamu.
Mlangoni hapo kulikuwa na mtungi mkubwa wa damu, kila mshirika aliyekuwa akiingia kanisa, ilikuwa ni lazima kuinama mlangoni kisha kuingia. Unapoinama pale mlangoni, unauinamia ule mtungi bila kujua na katika hali ambayo sikuifahamu, kuna kiasi kidogo cha damu unachangia katika mtungi ule.
Unajiona kwamba umevaa nguo lakini unapouvuka mlango wa kuingia kanisani, nguo zako zinaachwa mlangoni na wewe kuingia mtupu.
Kanisani mule hakukuwa na washirika tu bali kulikuwa na viumbe vingine vya ajabu ambavyo kazi zao zilikuwa zilezile za kuwavuta watu. Viumbe hivyo vya ajabu havikuwa ndani ya kanisa tu bali vilikuwepo mpaka pale nje.
Ushawahi kupita nje ya kanisa fulani, unasikia kuwa na hamu ya ghafla kuingia kanisani humo kwa ajili ya kuabudu? Yaani moyo wako unakusisimka na kutamani zaidi uingie. Ndugu yangu, hiyo inakuwa ni kazi ya hivyo viumbe vya ajabu ambavyo husimama nje na kukuvuta wewe.
Nilimuona mchungaji yule akiwaombea watu, mkononi alikuwa na kitambaa cheupe, kazi yake kubwa ilikuwa ni kuwapiga watu na kile kitambaa ambacho Yusnath aliniambia kwamba kilikuwa chao na walimpa kwa ajili ya kufanyia kazi hiyo.
Mtu anapopigwa na kitambaa kile, kwanza akili yake inachanganyikiwa, hakuna kitu kingine anachokipenda zaidi ya kuingia kanisani humo na huwa mtumwa wa moja kwa moja.
Mambo niliyokuwa nikiyaona ndani ya kanisa lile yalinishtua sana. Pembeni ya kiti cha mchungaji kulikuwa na joka kubwa, kazi yake ilikuwa ni kukaa hapohapo huku akiwaangalia washirika.
Ukiachana na joka lile, kulikuwa na joka jingine ambalo lilikuwa likitembea huku na kule, kazi yake kubwa ilikuwa ni kuwatemea watu mate ambayo Yusnath aliniambia kwamba mara unapotemewa mate yale, hata kama kuna mtu atakuja na kukwambia yule mchungaji ni mchawi, mzinzi, huwezi kuamini na unaweza kugombana na mtoa taarifa.
“Kumbeeee....” nilisema.
“Kumbe nini?”
“Nilipokuwa nikipita nje ya kanisa lake nilitamani kuingia,” nilimwambia.
“Hiyo ndiyo kazi ya vile viumbe, kuwavuta nyie tu.”
“Sawa. Kuna kingine?”
Hakutaka kuniambia hivihivi tu, alitaka kunionyeshea kila kitu kupitia televisheni ile. Nilimuona mchungji akichukua mafuta fulani hivi, alijipaka mikononi, alipokuwa akimuona mshirika mwanamke mzuri, alikuwa akimfuata na kumpaka mafuta yale na kumwambia kwamba yalitoka kwa Mungu kumbe hakuna lolote lile.
Baada ya kupakwa mafuta yale, akili ya msichana huyo inachanganyikiwa, muda mwingi anamuwaza mchungaji na mwisho wa siku kulala naye kitanda kimoja.
Kila nilichokuwa nikikiangalia, kilinifanya nichukie, nilikuwa mkristo, lakini sikuwa mtu wa kwenda kanisani lakini yale yaliyokuwa yakifanywa kwa baadhi ya makanisa likiwepo lile la mchungaji huyu, lilinisikitisha sana.
“Unajua watu wanaponywa vipi magonjwa yao?” aliniuliza Yusnath.
“Hapana! Inakuwaje?”
“Njoo huku,” aliniambia, akanishika mkono na kuanza kuelekea katika chumba kimoja.
Kilikuwa kikitisha sana, kulikuwa na maiti nyingi zilizokuwa zimetobolewatobolewa, sikujua na nini lakini nyingine zilivarishwa sanda nyeupe kabisa zisizokuwa na doa hata kidogo.
Chumbani mule kulikuwa na milio ya ajabu, wakati mwingine ilisikika milio ya paka lakini wakati mwingine ya bundi, kila nilipoisikia, niliogopa sana. Yusnath hakutaka kujali, aliendelea kunishika mkono na kuelekea mbele zaidi huku sakafuni kukiwa na damu nyingi zilizokuwa zikinuka mno.
Tukafika sehemu moja iliyokuwa na uwanja mkubwa, sikujua kama ilikuwa makaburini au la, alichoniambia ni kwamba nisimame imara, nikatii, akaniambia kwamba kuna mambo mengine ya mtume huyo nitayaona, nikamwambia hakuna tatizo, hivyo nikaanza kusubiri huku mwili ukinisisimka mno kwani sehemu ile ilitisha sana.
Je nini kitaendelea?
Tukutane Jumatatu mahali hapa.
Tukutane Jumatatu mahali hapa.
No comments:
Post a Comment