SIMULIZI YA KWELI: NILIONGEA NA SHETANI NIWE TAJIRI
NA: STALLONE JOYFULLY
NA: STALLONE JOYFULLY
SEHEMU YA NNE
aliniambia huku akiwa na anatokwa na machozi ya damu. Sikuelewa hali hiyo
ilimaanisha nini ila nilishindwa kukubali haraka haraka. Lakini pia
sikupenda kufa mapema kama alivyokufa mama. Nilitambua fika ule ndio
ulikuwa mwisho wa kuonana na mama yangu. Mama aliondoka katikati yetu na
kuvalishwa kaniki nyeusi kama walizovaa wengine wengi katika kjiji
hicho. Baada
ya kutafakari sana kwa dakika chache baadaye nilimjibu babu. "babu naogopa
kuwa mchawi" Nilijibu kiuwoga. Nilijibu nikiwa namaanisha kweli ninaogopa
kuwa mchawi. Tuliendelea kutembea katika mitaa mbalimbali ya kijiji hiko
cha wachawi.
Babu alitabasamu na kunigeukia "mjukuu wangu uchawi hauna madhara yoyote"
"babu hauna madhara?" Niliuliza kwa mshituko. Babu alicheka na kunijibu
kifupi
"ndiyo, hauna madhara yoyote"
"babu mimi siwezi kula nyama ya mtu, kunywa damu ya binadamu wala mnyama,
siwezi kuua. Babu sitaki kuwa mchawi"
babu alizungumza na mimi kwa upendo hata nikajisikia faraja
"mjukuu wangu, nafasi niliyo nayo ni kuwaadhibu wale wanaokiuka masharti ya
mkuu wa ulimwengu huu hivyo wewe nawe utakuwa vivyo hivyo kama utakubali
kurithi nafasi yangu"
nilimuomba babu anipe muda nitafakari jambo hilo kwa muda. Babu alinipa
masaa machache hivyo alidai kuwa angelifuata jibu lake usiku. Tulipokuwa
tukiendelea kutembea tembea, nilishituka kumuona mtu ninayemfahamu kabisa.
Alikuwa ni mtu mmoja maarufu huko duniani. Alikuwa ni mwanasiasa
aliyeogopwa sana na vyama pinzani, pamoja na chama chake. Nilisikitika
kumuona akiwa pale. Amechoka, amekuwa mweusi tofauti na alivyokuwa kule
duniani. Nilipotaka kuzungumza naye, babu alinizuia.
"hapana Bella, wewe bado hujawa na nguvu za kuweza kuzungumza na misukule"
nikamuuliza babu "kwani huyu amefanya nini mpaka yupo mahali hapa?"
"yeye alitolewa kafara na mume wake, mume wake ni mfanyabiashara maarufu
lakini yupo katika chama kimoja maarufu kinachotoa kafara na kumwaga damu
kwa sababu ya utajiri"
nilitetemeka sana niliposikia hivyo. Baada ya muda, nikatamani kuzunguka
zunguka tu mule katika kile kjiji cha Gamboshi ili niweze kuwaona watu
mbalimbali ambao ninawafahamu.
Tulipita katika kijiji duni ambacho niliwaacha wale misukule sasa tukaingia
katika sehemu yenye uafadhali wa maisha katika shemu hiyo ya Gamboshi.
Babu alinieleza "kule tulipopita mwanzo, ndipo wanapoishi misukule. Lakini
huku ndipo ilipo ngome yangu na wachawi wengine wakubwa huko duniani."
mbele ya majumba mbalimbali ya kifahari. Yaliyojengwa kiufahari. Niliuona
mji Fulani ulikuwa uking'aa sana. Ulikuwa ni mji uliokuwa ukiwaka taa
zilizotowa mwanga mkali hata kufanya niuone mji ule ukipendeza sana.
Nikamuuliza babu "kule ni wapi na kuna nini?" Babu hakunijibu kitu na
kunieleza ile si sehemu nzuri kuifikiria wala kutamani kwenda. Alinieleza,
miaka mingi sana iliyopita ufalme wa falme ile ilijaribu kutaka kupindua
tawala ya mkuu wao na kushindwa. hivyo ilijitenga nao na kuwa maadui
wakubwa baada ya urafiki uliokithiri na kujikita katika ndani ya mishipa
yao ya damu kabisa, kupoteza mvuto. Sikutaka kuendelea kuuliza zaidi lakini
nilihisi jambo kuhusu mji ule niliouona. Mji ule na hapa Gamboshi tulipo,
kuliteganishwa na shimo moja refu liliokuwa likitokota uji mzito wa moto.
Tofauti ya mji ule na huu wa ngome ya babu ilipo. Japokuwa mji ule
ulipendeza na uling'aa sana lakini huu wa babu ulififia na kuwa kama wenye
giza Fulani lisiloeleweka. Babu alinitoa hapo na kunionesha sehemu ambayo
mkuu wao alikuwa akiishi. Alinieleza "mjukuu wangu, sehemu hii ni takatifu
sana. Watu wote maarufu uwajuao huko duniani, huja mahali hapa kumuomba
mkuu wetu utajiri na kusafisha nyota zao ili waweze kukubalika zaidi na
zaidi."
"ninaweza kumuona?"
niliuliza
"hapana, bado hujafikia viwango vya kukanyaga sehemu ile" tuliondoka mahali
hiyo na kurudi kule kwa awali. Kule kulipochosha. Kule niliposhuhudia
misukule ikifanya kazi kwa bidii. Kule ambapo naamini ningemuona tena mama
na nimuage kuwa ipo siku nitarudi kuja kumtoa. Nilimuuliza babu "hivi hawa
hufanya kazi kwa muda gani" Babu alicheka sana na kunieleza kuwa "hawana
mapumziko, hufanya kazi usiku na mchana na hupumzika mara moja tu kwa siku"
alinyamaza baada ya kumeza mate kasha aliendelea kunieleza "wakati ambao
umepangwa wa wao kula tu"
"na huwa wanakula nini?" akanijibu "unga na funza, ndio chakula chao kikuu"
nilishangaa sana, ghafla machozi yalinitoka. Nilihuzunika kwa kuwa
nilifahamu mama yangu naye alikwisha kuwa msukule. Hivyo chakula chake
nacho kingekuwa ni hicho hicho. Nilimlaumu babu kwanini alimuuwa mama
yangu. Nililia kwa uchungu huku nikikimbia kusikojulikana. Nilikuwa sijuhi
wapi naenda ila nilipishana na misukule na vile viumbe vilivyopaa kama
ndege lakini wakiwa na maumbo ya binadamu. Ghafla Mbele yangu nilikutana
babu akinicheka kwa sauti ya juu sana. Aliniambia "Bella huku huna pa
kunikimbia" nilimjibu "babu nakuchukia, nakuchukia kuliko navyomchukia
shetani"
ghafla babu alinipiga kibao kilichonifanya nipoteze fahamu. Fahamu
iliyonitoa katika ulimwengu wa Gamboshi na kunirudisha duniani. Nilijikuta
nikiwa katikati ya watu wengi. Watu waliokuwa wakilia wakinamama
wamejifunga kanga zao. Wengine wakinipepea huku wakilia kwa uchungu
wakiliita jina la mama yangu.
niliposhituka nilipiga chafya mara tatu mfululizo. Watu walijawa na
mshituko. Niliwaona wengi wakiwa na maswali mengi sana juu ya kifo cha
mama. Mimi pia nilianza kulia kwa uchungu. Nilifahamu fika sitoweza kumuona
tena mama yangu katika ulimwengu huu wa kawaida. Watu walinibembeleza
lakini niliona kama walikuwa wakiniongezea uchungu zaidi. Walimuita Mzee
Nyegezi. Mzee Nyegezi alikuwa akizungumza na askari polisi waliofika eneo
la nyumbani kwetu. Watu walikuwa wamejaa sana. Hakika kifo cha mama
kilishitua wengi. Mzee Nyegezi na wale askari, walisubiri ninyamaze kulia
kisha waniulize maswali kadhaa. "pole sana binti" Alizungumza askari mmoja
aliyevalia sare zake.
"salama" kwikwi ilinibana, lakini nilijibu hivyo hivyo. Wakati huo huo
ambao askari wakiendelea kuzungumza, ghafla niliisikia sauti ya babu yangu
ikizungumza na nafsi yangu
"usiwaeleze chochote askari kuhusu kifo cha mama yako, wajibu hufahamu kitu"
nilipopata kigugumizi cha kujibu kutokana na sauti niliyoisikia, macho
yangu yakapata mshangao zaidi nilipomuona babu mbele yangu. Alikuwa kwenye
msiba huo kama waombolezaji wengine wa kawaida. "unaweza kutueleza
chochote ulichokiona?"
askari mmoja akalirudia Swali aliloliuliza zaidi ya mara tatu. Sikulisikia
kutokana na uwoga na nilijifanya sikuliskia kwa kuwa jibu walilotaka sikuwa
tayari kuwajibu.
walinipa muda wa kupumzika zaidi. Huku nikisikia kuwa, mwili wa mama upo
hospitali kwa ajili ya uchunguzi. Bado nilikuwa katika woga zaidi. Watu
mbalimbali waliingia katika chumba nilichomo kunipa pole. Nilimuona Jordan
mpenzi wangu. Nilimuona Bertha rafiki yangu na wanafunzi wenzangu wa
shuleni. Dakika chache baadae aliingia mwanamke fulani mwenye mwili mpana
na uso wa mviringo. Uwazi Fulani katikati ya meno yake ukamfanya awe na
mwanya hata akapendezesha kwa jino la dhahabu. Alijitanda kanga juu, chini
akakivaa kitenge kutoka kongo.
sikuwahi kumuona hata siku moja. Aliniambia "pole sana Bella" Nilikuwa
nikimtazama kwa makini bila kukumbuka ni wapi niliwahi kumuona. Nilimjibu
"asante, sijuhi niliwahi kukuona wapi?" akanijibu. "Gamboshi," hapo hapo
nilipoteza fahamu na kuisalimia sakafu kwa kuibusu. Dakika chache baadaye
niliamka kutoka usingizini. Nilijikuta katikati ya kundi kubwa la watu
wakinisikitikia. Kila mmoja alisema lake
"kufiwa na mama si kitu cha mchezo"
"tena kuna tetesi alikuwa naye" mwingine alisema "mama yake amekufa kifo
cha kinyama sana" Nikaanza tena kulia kwa uchungu. Nililia sana kwa sababu
nilifahamu fika chanzo na sababu ya kufa kwa mama yangu ni kuzuia harakati
za babu mimi kuwa mchawi. Nikiwa katika kulia huko sikujua nilipata hisia
gani hata zikanigusa nitazame nyuma ya mlango wa chumba nilichomo.
Nilimuona mama akiwa hana uwezo wowote wa kuongea.
Nilizidi kulia. Mbele yangu akatokea babu na kunieleza kuwa. "sasa umeweza
kuwa mchawi" Nilishituka sana. Sikujuwa ilikuwaje nikawa mchawi bila
kukubali mwenyewe na ilikuwa saa ngapi nikawa mchawi. Babu aliongea na
mimi bila mtu yeyote kufahamu kama nilikuwa nikizungumza na babu
"uliniambia nikupe jibu jioni kama nimekubali, imekuwaje uniambie nimekuwa
mchawi sasa?" Alicheka sana kisha aliniambia
"mjukuu wangu unatamani utajiri na nyota yako inawaka sana"
"hujajibu swali langu babu"
"ipo siku utanielewa acha tuyamalize haya ya msiba kwanza"
alipotaka kutoweka mbele yangu nilizishangaa nguvu nilizonazo. Niliweza
kumzuia.
"mama anafanya nini hapa?"
nilimuuliza huku nikiangalia eneo la mlangoni. Babu naye aligeuka kuangalia
alipo mama. Alinigeukia huku akitabasamu kifedhuli na kuniambia
"atakaa pale mpaka mtakapomsalia katika mazishi yake. Ule mwili ambao
wameenda kuufanyia uchunguzi si mwili bali ni mgomba. Usiogope, hana uwezo
wa kufanya lolote pale na hakuna anayemuona"
nilisonya kwa hasira na babu alitoweka hapo hapo. Nilisonya kiasi kwamba,
hata waombolezaji wengine walishituka. Mama mmoja aliniuliza "kuna nini
Bella?"
nilitingisha kichwa nikikataa kuwa hakuna kilichotokea. Nikatoka nje,
nilishangaa kumkuta babu akiwa pale pale nilipomuona mchana akiwa na wale
askari pamoja na Mzee Nyegezi. Mzee Nyegezi naye alinifuata na
kuniuliza "unajisikiaje
sasa Bella" nilimjibu tu, ilimradi
"vizuri" akaniuliza "Nyama ya mama yako ni tamu?" alikuwa akinichekea kwa
kunikejeli. Akaamsha hasira zangu. Nilimuangalia Mzee Nyegezi kwa jicho la
chuki hata nikamuona akianza kutokwa na jasho jingi sana. Nilijihisi nikiwa
na nguvu za ajabu, nguvu za kumuadhibu yeyote kwa kumtazama tu. Ilikuwa
inashangaza.
Muda wote huo babu alikuwa akinitazama. Alikuwa akitabasamu kwa raha sana.
Nilimuona Mzee Nyegezi akilalamika. "Bella unaniunguza na macho yako". Nikampa
onyo
"ole wako umueleze yeyote kuhusu msiba wa mama"
"nisamehe Bella usiniadhibu sintomueleza yeyote"
taratibu za mazishi ziliendeshwa na famila ya mama mkubwa. Ndugu na
marafiki wa mama walijumuika pamoja kumsindikiza mama katika safari yake ya
mwisho. Watu walikuwa ni wengi sana. Siwezi kusema kuwa nilihesabu idadi
yao, kwasababu nisingeweza. Misa takatifu ya kumuombea mama, ilifanyika
katika kanisa la katoliki mule mule ndani ya hospitali ya muhimbili.
Nilishituka kumuona yule mama aliyenitokea mule chumbani kichawi, akiwa
kwenye madhabahu huku akitoa maelekezo
"mwili wa mama yake Bella hautafunuliwa kutoka katika jeneza lake kutokana
na wingi wa watu pamoja na kifo alichokufa. Hivyo tumeamua kuweka picha tu
ambayo mtapita mkitoa heshima zenu za mwisho kwa kupita njia hii na
kuelekea nje ambapo kuna magari ya kuwapeleka makaburini." Nilimgeukia Mzee
Nyegezi aliye pembeni yangu, nikamuuliza
"hivi huyu mama ni nani?"
"nimetambulishwa na babu yako kuwa ni ndugu wa mama yako"
"na babu si ni baba wa baba yangu? Imekuwaje yeye afahamu ndugu wa mama
yangu?"
"sifahamu Bella naomba uniache kidogo"
tulienda kuaga kwa taratibu tulizoelekezwa na yule mama. Nilijaribu
kumtafuta, lakini sikumuona tena eneo hilo la msiba. Mpaka tulipoingizwa
kwenye magari ya kuelekea makaburini kuuzika mwili wa mama.
Baada ya mazishi tulirudi nyumbani. Baada ya siku chache baadaye, msiba
ulipomalizika maisha yalikuwa shwari wala babu na yule mama wa maajabu
hawakutokea tena. Siku moja nikiwa shuleni pamoja na rafiki zangu, alikuja
Berther na kunieleza kuwa "kuna mtu kule nje anakuita" nikamuuliza
"mwanamke mwanaume?"
"mmama mmoja hivi, ila niliwahi kumuona msibani kwenu"
mimi nilitoka mbio mpaka getini kumtazama huyo mama. Mawazo yalijua fika ni
yule mjumbe wa wachawi kutoka Gamboshi. Alifuata nini kwangu? alitaka nini?
Nilipofika getini, sikukuta mtu. Nilipotaka kugeuza na kurudi ndani.
Nilimuona babu amesimama pembeni ya ukuta wa shule akicheka "vipi mbona una
wasiwasi?" aliniuliza ghafla. "babu yule mwanamke ni nani?" nilifahamu
fika anafahamu ninachozungumzia. Alicheka bila kunipa jibu lolote.
Nikamuuliza tena "umekuja kufanya nini hapa?" alinijibu "nataka ukadhuru
Gamboshi mara ya mwisho kabla hujarithi kiti changu" moyo wangu ukaanza
kwenda mbio sana. Ghafla mbele yetu tuliposimama, lilikuja gari la maajabu
na ndani yake abiria walikuwa uchi wa mnyama. Nikisema gari la maajabu,
namaanisha gari lile lilipita eneo la shule bila hata kufunguliwa geti na
wala hakukuwa na barabara eneo hilo. Tulielekea gamboshi. Tulipoingia ndani
ya lile gari la kichawi, sikuwa muoga tena. Niliwaona watu walio nadhifu
kimavazi kuonesha walikuwa na uafadhali wa kifedha. Watu hao walijitundika
ndani ya suti nyeusi mikononi walizibeba biblia. Nikajinong'oneza
"wachungaji?" nilishituka sana. Ilibidi, nimuulize babu. "hawa si watumishi
wa mungu?" Babu alinipiga kibao kikali sana na kunikataza kwa kuniambia
kuwa, jina hilo halikuruhusiwa kutajwa eneo lile. Kisha aliniambia kuwa
"hawa si watumishi wa huyo anayedhaniwa kuwa aliwaumba binadamu"
nilimeza mate nikiugulia maumivu huku nikiwaangalia wale watu waliokuwa
kimya muda wote. "sasa huku Gamboshi, wanaenda kufanya nini?"
Babu alicheka kicheko kisicho na ladha ya kuitwa kicheko. Kisha aliniambia
kuwa
"hawa ni wachungaji maarufu sana huko duniani wanaolihubiri jina la mkuu
wetu kupitia hizo dini zao. wachache huwafahamu kama wakiwa pamoja nasi
katika ulimwengu huu wa Gamboshi" Nilikuwa nimetumbua macho muda wote.
hakika ilikuwa habari ya kushangaza na kutisha muda wote. Kisha babu
aliendelea kuniambia. "wengi wamepata nguvu ya uponyaji kutoka kwa mkuu
wetu. Unapoponywa na mmoja kati ya wachungaji hawa, lazima wewe uwe mmoja
wa wanachama wa kuleta watu wengine wengi katika ulimwengu wa mkuu wetu."
sasa ndio nikakumbuka mama aliwahi kuniambia mwisho wa dunia yatatokea
mambo mengi ya kutisha na kushangaza. Manabii wengi wa uongo wataponya.
viwete wakatembea, viziwi wakasikia na mabubu kupiga yowe; nikiona ishara
hizo nisihangaike katika kukimbilia miujiza nisimamie imani yangu. Mwili
wangu ukasisimka hata vinyweleo vikasimama. Nilimgeukia babu na kumuuliza.
"mbona gari imesimama na hawa wanashuka?" babu alinieleza kuwa "hawa ni
wachawi ambao wanaenda kuongezewa vyeo kwa kazi walizofanya bada ya kutumwa
na kuzifanikisha. Hupewa fisi wa kutembelea ama mnyama yeyote. Hongezewa
nguvu pia kwa kujilinda na maadui na nguvu za walokole"
ilimaanisha nini ila nilishindwa kukubali haraka haraka. Lakini pia
sikupenda kufa mapema kama alivyokufa mama. Nilitambua fika ule ndio
ulikuwa mwisho wa kuonana na mama yangu. Mama aliondoka katikati yetu na
kuvalishwa kaniki nyeusi kama walizovaa wengine wengi katika kjiji
hicho. Baada
ya kutafakari sana kwa dakika chache baadaye nilimjibu babu. "babu naogopa
kuwa mchawi" Nilijibu kiuwoga. Nilijibu nikiwa namaanisha kweli ninaogopa
kuwa mchawi. Tuliendelea kutembea katika mitaa mbalimbali ya kijiji hiko
cha wachawi.
Babu alitabasamu na kunigeukia "mjukuu wangu uchawi hauna madhara yoyote"
"babu hauna madhara?" Niliuliza kwa mshituko. Babu alicheka na kunijibu
kifupi
"ndiyo, hauna madhara yoyote"
"babu mimi siwezi kula nyama ya mtu, kunywa damu ya binadamu wala mnyama,
siwezi kuua. Babu sitaki kuwa mchawi"
babu alizungumza na mimi kwa upendo hata nikajisikia faraja
"mjukuu wangu, nafasi niliyo nayo ni kuwaadhibu wale wanaokiuka masharti ya
mkuu wa ulimwengu huu hivyo wewe nawe utakuwa vivyo hivyo kama utakubali
kurithi nafasi yangu"
nilimuomba babu anipe muda nitafakari jambo hilo kwa muda. Babu alinipa
masaa machache hivyo alidai kuwa angelifuata jibu lake usiku. Tulipokuwa
tukiendelea kutembea tembea, nilishituka kumuona mtu ninayemfahamu kabisa.
Alikuwa ni mtu mmoja maarufu huko duniani. Alikuwa ni mwanasiasa
aliyeogopwa sana na vyama pinzani, pamoja na chama chake. Nilisikitika
kumuona akiwa pale. Amechoka, amekuwa mweusi tofauti na alivyokuwa kule
duniani. Nilipotaka kuzungumza naye, babu alinizuia.
"hapana Bella, wewe bado hujawa na nguvu za kuweza kuzungumza na misukule"
nikamuuliza babu "kwani huyu amefanya nini mpaka yupo mahali hapa?"
"yeye alitolewa kafara na mume wake, mume wake ni mfanyabiashara maarufu
lakini yupo katika chama kimoja maarufu kinachotoa kafara na kumwaga damu
kwa sababu ya utajiri"
nilitetemeka sana niliposikia hivyo. Baada ya muda, nikatamani kuzunguka
zunguka tu mule katika kile kjiji cha Gamboshi ili niweze kuwaona watu
mbalimbali ambao ninawafahamu.
Tulipita katika kijiji duni ambacho niliwaacha wale misukule sasa tukaingia
katika sehemu yenye uafadhali wa maisha katika shemu hiyo ya Gamboshi.
Babu alinieleza "kule tulipopita mwanzo, ndipo wanapoishi misukule. Lakini
huku ndipo ilipo ngome yangu na wachawi wengine wakubwa huko duniani."
mbele ya majumba mbalimbali ya kifahari. Yaliyojengwa kiufahari. Niliuona
mji Fulani ulikuwa uking'aa sana. Ulikuwa ni mji uliokuwa ukiwaka taa
zilizotowa mwanga mkali hata kufanya niuone mji ule ukipendeza sana.
Nikamuuliza babu "kule ni wapi na kuna nini?" Babu hakunijibu kitu na
kunieleza ile si sehemu nzuri kuifikiria wala kutamani kwenda. Alinieleza,
miaka mingi sana iliyopita ufalme wa falme ile ilijaribu kutaka kupindua
tawala ya mkuu wao na kushindwa. hivyo ilijitenga nao na kuwa maadui
wakubwa baada ya urafiki uliokithiri na kujikita katika ndani ya mishipa
yao ya damu kabisa, kupoteza mvuto. Sikutaka kuendelea kuuliza zaidi lakini
nilihisi jambo kuhusu mji ule niliouona. Mji ule na hapa Gamboshi tulipo,
kuliteganishwa na shimo moja refu liliokuwa likitokota uji mzito wa moto.
Tofauti ya mji ule na huu wa ngome ya babu ilipo. Japokuwa mji ule
ulipendeza na uling'aa sana lakini huu wa babu ulififia na kuwa kama wenye
giza Fulani lisiloeleweka. Babu alinitoa hapo na kunionesha sehemu ambayo
mkuu wao alikuwa akiishi. Alinieleza "mjukuu wangu, sehemu hii ni takatifu
sana. Watu wote maarufu uwajuao huko duniani, huja mahali hapa kumuomba
mkuu wetu utajiri na kusafisha nyota zao ili waweze kukubalika zaidi na
zaidi."
"ninaweza kumuona?"
niliuliza
"hapana, bado hujafikia viwango vya kukanyaga sehemu ile" tuliondoka mahali
hiyo na kurudi kule kwa awali. Kule kulipochosha. Kule niliposhuhudia
misukule ikifanya kazi kwa bidii. Kule ambapo naamini ningemuona tena mama
na nimuage kuwa ipo siku nitarudi kuja kumtoa. Nilimuuliza babu "hivi hawa
hufanya kazi kwa muda gani" Babu alicheka sana na kunieleza kuwa "hawana
mapumziko, hufanya kazi usiku na mchana na hupumzika mara moja tu kwa siku"
alinyamaza baada ya kumeza mate kasha aliendelea kunieleza "wakati ambao
umepangwa wa wao kula tu"
"na huwa wanakula nini?" akanijibu "unga na funza, ndio chakula chao kikuu"
nilishangaa sana, ghafla machozi yalinitoka. Nilihuzunika kwa kuwa
nilifahamu mama yangu naye alikwisha kuwa msukule. Hivyo chakula chake
nacho kingekuwa ni hicho hicho. Nilimlaumu babu kwanini alimuuwa mama
yangu. Nililia kwa uchungu huku nikikimbia kusikojulikana. Nilikuwa sijuhi
wapi naenda ila nilipishana na misukule na vile viumbe vilivyopaa kama
ndege lakini wakiwa na maumbo ya binadamu. Ghafla Mbele yangu nilikutana
babu akinicheka kwa sauti ya juu sana. Aliniambia "Bella huku huna pa
kunikimbia" nilimjibu "babu nakuchukia, nakuchukia kuliko navyomchukia
shetani"
ghafla babu alinipiga kibao kilichonifanya nipoteze fahamu. Fahamu
iliyonitoa katika ulimwengu wa Gamboshi na kunirudisha duniani. Nilijikuta
nikiwa katikati ya watu wengi. Watu waliokuwa wakilia wakinamama
wamejifunga kanga zao. Wengine wakinipepea huku wakilia kwa uchungu
wakiliita jina la mama yangu.
niliposhituka nilipiga chafya mara tatu mfululizo. Watu walijawa na
mshituko. Niliwaona wengi wakiwa na maswali mengi sana juu ya kifo cha
mama. Mimi pia nilianza kulia kwa uchungu. Nilifahamu fika sitoweza kumuona
tena mama yangu katika ulimwengu huu wa kawaida. Watu walinibembeleza
lakini niliona kama walikuwa wakiniongezea uchungu zaidi. Walimuita Mzee
Nyegezi. Mzee Nyegezi alikuwa akizungumza na askari polisi waliofika eneo
la nyumbani kwetu. Watu walikuwa wamejaa sana. Hakika kifo cha mama
kilishitua wengi. Mzee Nyegezi na wale askari, walisubiri ninyamaze kulia
kisha waniulize maswali kadhaa. "pole sana binti" Alizungumza askari mmoja
aliyevalia sare zake.
"salama" kwikwi ilinibana, lakini nilijibu hivyo hivyo. Wakati huo huo
ambao askari wakiendelea kuzungumza, ghafla niliisikia sauti ya babu yangu
ikizungumza na nafsi yangu
"usiwaeleze chochote askari kuhusu kifo cha mama yako, wajibu hufahamu kitu"
nilipopata kigugumizi cha kujibu kutokana na sauti niliyoisikia, macho
yangu yakapata mshangao zaidi nilipomuona babu mbele yangu. Alikuwa kwenye
msiba huo kama waombolezaji wengine wa kawaida. "unaweza kutueleza
chochote ulichokiona?"
askari mmoja akalirudia Swali aliloliuliza zaidi ya mara tatu. Sikulisikia
kutokana na uwoga na nilijifanya sikuliskia kwa kuwa jibu walilotaka sikuwa
tayari kuwajibu.
walinipa muda wa kupumzika zaidi. Huku nikisikia kuwa, mwili wa mama upo
hospitali kwa ajili ya uchunguzi. Bado nilikuwa katika woga zaidi. Watu
mbalimbali waliingia katika chumba nilichomo kunipa pole. Nilimuona Jordan
mpenzi wangu. Nilimuona Bertha rafiki yangu na wanafunzi wenzangu wa
shuleni. Dakika chache baadae aliingia mwanamke fulani mwenye mwili mpana
na uso wa mviringo. Uwazi Fulani katikati ya meno yake ukamfanya awe na
mwanya hata akapendezesha kwa jino la dhahabu. Alijitanda kanga juu, chini
akakivaa kitenge kutoka kongo.
sikuwahi kumuona hata siku moja. Aliniambia "pole sana Bella" Nilikuwa
nikimtazama kwa makini bila kukumbuka ni wapi niliwahi kumuona. Nilimjibu
"asante, sijuhi niliwahi kukuona wapi?" akanijibu. "Gamboshi," hapo hapo
nilipoteza fahamu na kuisalimia sakafu kwa kuibusu. Dakika chache baadaye
niliamka kutoka usingizini. Nilijikuta katikati ya kundi kubwa la watu
wakinisikitikia. Kila mmoja alisema lake
"kufiwa na mama si kitu cha mchezo"
"tena kuna tetesi alikuwa naye" mwingine alisema "mama yake amekufa kifo
cha kinyama sana" Nikaanza tena kulia kwa uchungu. Nililia sana kwa sababu
nilifahamu fika chanzo na sababu ya kufa kwa mama yangu ni kuzuia harakati
za babu mimi kuwa mchawi. Nikiwa katika kulia huko sikujua nilipata hisia
gani hata zikanigusa nitazame nyuma ya mlango wa chumba nilichomo.
Nilimuona mama akiwa hana uwezo wowote wa kuongea.
Nilizidi kulia. Mbele yangu akatokea babu na kunieleza kuwa. "sasa umeweza
kuwa mchawi" Nilishituka sana. Sikujuwa ilikuwaje nikawa mchawi bila
kukubali mwenyewe na ilikuwa saa ngapi nikawa mchawi. Babu aliongea na
mimi bila mtu yeyote kufahamu kama nilikuwa nikizungumza na babu
"uliniambia nikupe jibu jioni kama nimekubali, imekuwaje uniambie nimekuwa
mchawi sasa?" Alicheka sana kisha aliniambia
"mjukuu wangu unatamani utajiri na nyota yako inawaka sana"
"hujajibu swali langu babu"
"ipo siku utanielewa acha tuyamalize haya ya msiba kwanza"
alipotaka kutoweka mbele yangu nilizishangaa nguvu nilizonazo. Niliweza
kumzuia.
"mama anafanya nini hapa?"
nilimuuliza huku nikiangalia eneo la mlangoni. Babu naye aligeuka kuangalia
alipo mama. Alinigeukia huku akitabasamu kifedhuli na kuniambia
"atakaa pale mpaka mtakapomsalia katika mazishi yake. Ule mwili ambao
wameenda kuufanyia uchunguzi si mwili bali ni mgomba. Usiogope, hana uwezo
wa kufanya lolote pale na hakuna anayemuona"
nilisonya kwa hasira na babu alitoweka hapo hapo. Nilisonya kiasi kwamba,
hata waombolezaji wengine walishituka. Mama mmoja aliniuliza "kuna nini
Bella?"
nilitingisha kichwa nikikataa kuwa hakuna kilichotokea. Nikatoka nje,
nilishangaa kumkuta babu akiwa pale pale nilipomuona mchana akiwa na wale
askari pamoja na Mzee Nyegezi. Mzee Nyegezi naye alinifuata na
kuniuliza "unajisikiaje
sasa Bella" nilimjibu tu, ilimradi
"vizuri" akaniuliza "Nyama ya mama yako ni tamu?" alikuwa akinichekea kwa
kunikejeli. Akaamsha hasira zangu. Nilimuangalia Mzee Nyegezi kwa jicho la
chuki hata nikamuona akianza kutokwa na jasho jingi sana. Nilijihisi nikiwa
na nguvu za ajabu, nguvu za kumuadhibu yeyote kwa kumtazama tu. Ilikuwa
inashangaza.
Muda wote huo babu alikuwa akinitazama. Alikuwa akitabasamu kwa raha sana.
Nilimuona Mzee Nyegezi akilalamika. "Bella unaniunguza na macho yako". Nikampa
onyo
"ole wako umueleze yeyote kuhusu msiba wa mama"
"nisamehe Bella usiniadhibu sintomueleza yeyote"
taratibu za mazishi ziliendeshwa na famila ya mama mkubwa. Ndugu na
marafiki wa mama walijumuika pamoja kumsindikiza mama katika safari yake ya
mwisho. Watu walikuwa ni wengi sana. Siwezi kusema kuwa nilihesabu idadi
yao, kwasababu nisingeweza. Misa takatifu ya kumuombea mama, ilifanyika
katika kanisa la katoliki mule mule ndani ya hospitali ya muhimbili.
Nilishituka kumuona yule mama aliyenitokea mule chumbani kichawi, akiwa
kwenye madhabahu huku akitoa maelekezo
"mwili wa mama yake Bella hautafunuliwa kutoka katika jeneza lake kutokana
na wingi wa watu pamoja na kifo alichokufa. Hivyo tumeamua kuweka picha tu
ambayo mtapita mkitoa heshima zenu za mwisho kwa kupita njia hii na
kuelekea nje ambapo kuna magari ya kuwapeleka makaburini." Nilimgeukia Mzee
Nyegezi aliye pembeni yangu, nikamuuliza
"hivi huyu mama ni nani?"
"nimetambulishwa na babu yako kuwa ni ndugu wa mama yako"
"na babu si ni baba wa baba yangu? Imekuwaje yeye afahamu ndugu wa mama
yangu?"
"sifahamu Bella naomba uniache kidogo"
tulienda kuaga kwa taratibu tulizoelekezwa na yule mama. Nilijaribu
kumtafuta, lakini sikumuona tena eneo hilo la msiba. Mpaka tulipoingizwa
kwenye magari ya kuelekea makaburini kuuzika mwili wa mama.
Baada ya mazishi tulirudi nyumbani. Baada ya siku chache baadaye, msiba
ulipomalizika maisha yalikuwa shwari wala babu na yule mama wa maajabu
hawakutokea tena. Siku moja nikiwa shuleni pamoja na rafiki zangu, alikuja
Berther na kunieleza kuwa "kuna mtu kule nje anakuita" nikamuuliza
"mwanamke mwanaume?"
"mmama mmoja hivi, ila niliwahi kumuona msibani kwenu"
mimi nilitoka mbio mpaka getini kumtazama huyo mama. Mawazo yalijua fika ni
yule mjumbe wa wachawi kutoka Gamboshi. Alifuata nini kwangu? alitaka nini?
Nilipofika getini, sikukuta mtu. Nilipotaka kugeuza na kurudi ndani.
Nilimuona babu amesimama pembeni ya ukuta wa shule akicheka "vipi mbona una
wasiwasi?" aliniuliza ghafla. "babu yule mwanamke ni nani?" nilifahamu
fika anafahamu ninachozungumzia. Alicheka bila kunipa jibu lolote.
Nikamuuliza tena "umekuja kufanya nini hapa?" alinijibu "nataka ukadhuru
Gamboshi mara ya mwisho kabla hujarithi kiti changu" moyo wangu ukaanza
kwenda mbio sana. Ghafla mbele yetu tuliposimama, lilikuja gari la maajabu
na ndani yake abiria walikuwa uchi wa mnyama. Nikisema gari la maajabu,
namaanisha gari lile lilipita eneo la shule bila hata kufunguliwa geti na
wala hakukuwa na barabara eneo hilo. Tulielekea gamboshi. Tulipoingia ndani
ya lile gari la kichawi, sikuwa muoga tena. Niliwaona watu walio nadhifu
kimavazi kuonesha walikuwa na uafadhali wa kifedha. Watu hao walijitundika
ndani ya suti nyeusi mikononi walizibeba biblia. Nikajinong'oneza
"wachungaji?" nilishituka sana. Ilibidi, nimuulize babu. "hawa si watumishi
wa mungu?" Babu alinipiga kibao kikali sana na kunikataza kwa kuniambia
kuwa, jina hilo halikuruhusiwa kutajwa eneo lile. Kisha aliniambia kuwa
"hawa si watumishi wa huyo anayedhaniwa kuwa aliwaumba binadamu"
nilimeza mate nikiugulia maumivu huku nikiwaangalia wale watu waliokuwa
kimya muda wote. "sasa huku Gamboshi, wanaenda kufanya nini?"
Babu alicheka kicheko kisicho na ladha ya kuitwa kicheko. Kisha aliniambia
kuwa
"hawa ni wachungaji maarufu sana huko duniani wanaolihubiri jina la mkuu
wetu kupitia hizo dini zao. wachache huwafahamu kama wakiwa pamoja nasi
katika ulimwengu huu wa Gamboshi" Nilikuwa nimetumbua macho muda wote.
hakika ilikuwa habari ya kushangaza na kutisha muda wote. Kisha babu
aliendelea kuniambia. "wengi wamepata nguvu ya uponyaji kutoka kwa mkuu
wetu. Unapoponywa na mmoja kati ya wachungaji hawa, lazima wewe uwe mmoja
wa wanachama wa kuleta watu wengine wengi katika ulimwengu wa mkuu wetu."
sasa ndio nikakumbuka mama aliwahi kuniambia mwisho wa dunia yatatokea
mambo mengi ya kutisha na kushangaza. Manabii wengi wa uongo wataponya.
viwete wakatembea, viziwi wakasikia na mabubu kupiga yowe; nikiona ishara
hizo nisihangaike katika kukimbilia miujiza nisimamie imani yangu. Mwili
wangu ukasisimka hata vinyweleo vikasimama. Nilimgeukia babu na kumuuliza.
"mbona gari imesimama na hawa wanashuka?" babu alinieleza kuwa "hawa ni
wachawi ambao wanaenda kuongezewa vyeo kwa kazi walizofanya bada ya kutumwa
na kuzifanikisha. Hupewa fisi wa kutembelea ama mnyama yeyote. Hongezewa
nguvu pia kwa kujilinda na maadui na nguvu za walokole"
No comments:
Post a Comment