SIMULIZI YA KWELI: NILIONGEA NA SHETANI NIWE TAJIRI
NA: STALLONE JOYFULLY
NA: STALLONE JOYFULLY
SEHEMU YA TANO
"hawa ni wachungaji maarufu sana huko duniani wanaolihubiri jina la mkuu
wetu kupitia hizo dini zao. wachache huwafahamu kama wakiwa pamoja nasi
katika ulimwengu huu wa Gamboshi" Nilikuwa nimetumbua macho muda wote.
hakika ilikuwa habari ya kushangaza na kutisha muda wote. Kisha babu
aliendelea kuniambia. "wengi wamepata nguvu ya uponyaji kutoka kwa mkuu
wetu. Unapoponywa na mmoja kati ya wachungaji hawa, lazima wewe uwe mmoja
wa wanachama wa kuleta watu wengine wengi katika ulimwengu wa mkuu wetu."
sasa ndio nikakumbuka mama aliwahi kuniambia mwisho wa dunia yatatokea
mambo mengi ya kutisha na kushangaza. Manabii wengi wa uongo wataponya.
viwete wakatembea, viziwi wakasikia na mabubu kupiga yowe; nikiona ishara
hizo nisihangaike katika kukimbilia miujiza nisimamie imani yangu. Mwili
wangu ukasisimka hata vinyweleo vikasimama. Nilimgeukia babu na kumuuliza.
"mbona gari imesimama na hawa wanashuka?" babu alinieleza kuwa "hawa ni
wachawi ambao wanaenda kuongezewa vyeo kwa kazi walizofanya bada ya kutumwa
na kuzifanikisha. Hupewa fisi wa kutembelea ama mnyama yeyote. Hongezewa
nguvu pia kwa kujilinda na maadui na nguvu za walokole"
kisha aliendelea kunieleza kuwa, wale wachawi wanaelekea eneo ambalo
kulikuwa na joka kubwa lenye vichwa vitatu. Joka hilo, ni kubwa sana. Joka
linalotowa nguvu hiyo. Vichwa hivyo vina sura za binadamu zinazotisha. Kwa
mtu wa kawaida huwezi kuzitazama zaidi ya sekunde tano bila nguvu za
kichawi, utazimia au kufa kabisa. Babu aliponieleza hayo niliogopa sana.
Siwezi kueleza kiasi nilichoogopa lakini hata wewe nikusimuliaye hadithi
hii, bila shaka unatetemeka. Basi gari lilikuwa linaenda kwa kasi kama
treni ya umeme. Tulipofika eneo Fulani, mimi na babu tulishuka na wale
wachungaji waliendelea na safari.
nilimuuliza tena babu "kumbe kule bado kuna safari nyingine ndefu?"
Alinijibu "kule ndipo mwisho wa safari, kule ndipo alipo mkuu wetu, kule
ndipo nilipokuonesha siku ile ya kwanza na kukuelekeza ile ni sehemu
takatifu sana. Ipo siku utakwenda ukishakuwa na nguvu za kutosha na
kukabidhi madaraka niliyonayo."
lile gari halikuchukuwa muda mrefu likawa limeshapotea machoni pangu. "sasa
mimi nimekuja kufanya nini huku ikiwa mimi bado sijawa mchawi?"
babu alicheka kama kawaida na kuniambia "wewe ni mchawi tayari ila huna
nguvu za kutosha za kukutana na mkuu wetu." Nilijiuliza mara kwa mara huyo
mkuu anayetajwa na babu sana, atakuwa ni nani? lakini sikupata jibu. Katika
kutembea na kuzuru eneo ambalo misukule walikuwa wakifanya kazi kulingana
na kazi zao au vipaji walivyokuwa navyo huko duniani, tuliingia katika
jengo moja ambalo babu aliniambia hiyo ni hospitali ya hapo Gamboshi.
Niliuliza
kwa mshangao "Hospitali? Kwani huku nako watu hupigania uhai?"
babu alinieleza " hiyo ni sehemu ya kubadilishana viungo baina ya misukule
na wachawi ambao huumizwa na nguvu za maombi ya walokole." Babu akanieleza
jambo moja ambalo hata leo silisahau "wachawi hawaogopi biblia wala jina
la huyo aliyekuja akasulubiwa msalabani(yesu) bali kwa hao wanaojifanya
wanaomfuata huyo mtu wao" hapa babu alinieleza kwa maneno ya kashfa sana.
Maneno ambayo yalimdhihaki Mungu. M Sikupenda niyaandike yote. Mara
nikamuona msukule ambaye alikuwa akifanyiwa jambo kama operasheni.
Alitolewa mguu na kubandikwa mtu mmoja aliyekuwa uchi akiugulia maumivu.
Babu alinieleza kuwa yule ni mchawi aliyevunjwa mguu na nguvu za maombi. Babu
akanigeukia na kunieleza "leo tutakuwa na safari ndefu kidogo huku
Gamboshi. Lakini isiyochosha. Leo ni siku ambayo utakabidhiwa utawala wangu
na utakuwa msichana wa kwanza tangu ulimwengu huu ulipoumbwa kwa kushika
nafasi kubwa kama hii. Mkuu wetu amependezwa na mg'ao wa nyota yako hivyo
ameamini akikutumia wewe atapata wafuasi wengi. Hakuna falme itakayoshinda
mara itakapojaribu kujiinua kupigana na wewe. Utakuwa msichana mwenye nguvu
za ajabu na utajiri usioelezeka. Ila kuna masharti utakayopewa ukiyatimiza
hayo utakuwa umenifurahisha sana."
Alinipiga piga mgongoni nikahisi kama nimeshikwa na nyaya za umeme.
Nilitetemeshwa.
Nilimuuliza babu nikiwa na tabasamu "babu sasa kwanini mkuu wenu ameamua
kunichagua mimi ikiwa bado mimi ni binti mdogo? Na nisiye na uwezo wowote
kifedha?"
"swali zuri sana. wakati wote nakueleza kuwa mkuu wetu amependezwa na nyota
yako hiyo ndio sababu iliyomvutia mkuu wetu" aliyameza mate kisha
aliniambia "mkuu wetu ana utajiri mkubwa yeye haihitaji sadaka" kisha babu
alicheka kifedhuli.
niliacha kuuliza maswali na kuendelea kuzuru Gamboshi kama mtalii. Nikaona
kikao kimoja klichohudhuriwa na watu wengi sana, kikiwa kinaongozwa na joka
kubwa yaani joka lile lilikuwa kubwa kupitiliza. Joka lile lilikuwa
likiwatemea wale watu mate yake. Cha ajabu mate yake yalikuwa mengi kila
alipokuwa akiwatemea ikawa kama ilikuwa inanyesha mvua. hivyo kila mmoja
aliye katika kikao kile alilowa chapachapa. babu alinieleza kuhusu joka
lile.
wetu kupitia hizo dini zao. wachache huwafahamu kama wakiwa pamoja nasi
katika ulimwengu huu wa Gamboshi" Nilikuwa nimetumbua macho muda wote.
hakika ilikuwa habari ya kushangaza na kutisha muda wote. Kisha babu
aliendelea kuniambia. "wengi wamepata nguvu ya uponyaji kutoka kwa mkuu
wetu. Unapoponywa na mmoja kati ya wachungaji hawa, lazima wewe uwe mmoja
wa wanachama wa kuleta watu wengine wengi katika ulimwengu wa mkuu wetu."
sasa ndio nikakumbuka mama aliwahi kuniambia mwisho wa dunia yatatokea
mambo mengi ya kutisha na kushangaza. Manabii wengi wa uongo wataponya.
viwete wakatembea, viziwi wakasikia na mabubu kupiga yowe; nikiona ishara
hizo nisihangaike katika kukimbilia miujiza nisimamie imani yangu. Mwili
wangu ukasisimka hata vinyweleo vikasimama. Nilimgeukia babu na kumuuliza.
"mbona gari imesimama na hawa wanashuka?" babu alinieleza kuwa "hawa ni
wachawi ambao wanaenda kuongezewa vyeo kwa kazi walizofanya bada ya kutumwa
na kuzifanikisha. Hupewa fisi wa kutembelea ama mnyama yeyote. Hongezewa
nguvu pia kwa kujilinda na maadui na nguvu za walokole"
kisha aliendelea kunieleza kuwa, wale wachawi wanaelekea eneo ambalo
kulikuwa na joka kubwa lenye vichwa vitatu. Joka hilo, ni kubwa sana. Joka
linalotowa nguvu hiyo. Vichwa hivyo vina sura za binadamu zinazotisha. Kwa
mtu wa kawaida huwezi kuzitazama zaidi ya sekunde tano bila nguvu za
kichawi, utazimia au kufa kabisa. Babu aliponieleza hayo niliogopa sana.
Siwezi kueleza kiasi nilichoogopa lakini hata wewe nikusimuliaye hadithi
hii, bila shaka unatetemeka. Basi gari lilikuwa linaenda kwa kasi kama
treni ya umeme. Tulipofika eneo Fulani, mimi na babu tulishuka na wale
wachungaji waliendelea na safari.
nilimuuliza tena babu "kumbe kule bado kuna safari nyingine ndefu?"
Alinijibu "kule ndipo mwisho wa safari, kule ndipo alipo mkuu wetu, kule
ndipo nilipokuonesha siku ile ya kwanza na kukuelekeza ile ni sehemu
takatifu sana. Ipo siku utakwenda ukishakuwa na nguvu za kutosha na
kukabidhi madaraka niliyonayo."
lile gari halikuchukuwa muda mrefu likawa limeshapotea machoni pangu. "sasa
mimi nimekuja kufanya nini huku ikiwa mimi bado sijawa mchawi?"
babu alicheka kama kawaida na kuniambia "wewe ni mchawi tayari ila huna
nguvu za kutosha za kukutana na mkuu wetu." Nilijiuliza mara kwa mara huyo
mkuu anayetajwa na babu sana, atakuwa ni nani? lakini sikupata jibu. Katika
kutembea na kuzuru eneo ambalo misukule walikuwa wakifanya kazi kulingana
na kazi zao au vipaji walivyokuwa navyo huko duniani, tuliingia katika
jengo moja ambalo babu aliniambia hiyo ni hospitali ya hapo Gamboshi.
Niliuliza
kwa mshangao "Hospitali? Kwani huku nako watu hupigania uhai?"
babu alinieleza " hiyo ni sehemu ya kubadilishana viungo baina ya misukule
na wachawi ambao huumizwa na nguvu za maombi ya walokole." Babu akanieleza
jambo moja ambalo hata leo silisahau "wachawi hawaogopi biblia wala jina
la huyo aliyekuja akasulubiwa msalabani(yesu) bali kwa hao wanaojifanya
wanaomfuata huyo mtu wao" hapa babu alinieleza kwa maneno ya kashfa sana.
Maneno ambayo yalimdhihaki Mungu. M Sikupenda niyaandike yote. Mara
nikamuona msukule ambaye alikuwa akifanyiwa jambo kama operasheni.
Alitolewa mguu na kubandikwa mtu mmoja aliyekuwa uchi akiugulia maumivu.
Babu alinieleza kuwa yule ni mchawi aliyevunjwa mguu na nguvu za maombi. Babu
akanigeukia na kunieleza "leo tutakuwa na safari ndefu kidogo huku
Gamboshi. Lakini isiyochosha. Leo ni siku ambayo utakabidhiwa utawala wangu
na utakuwa msichana wa kwanza tangu ulimwengu huu ulipoumbwa kwa kushika
nafasi kubwa kama hii. Mkuu wetu amependezwa na mg'ao wa nyota yako hivyo
ameamini akikutumia wewe atapata wafuasi wengi. Hakuna falme itakayoshinda
mara itakapojaribu kujiinua kupigana na wewe. Utakuwa msichana mwenye nguvu
za ajabu na utajiri usioelezeka. Ila kuna masharti utakayopewa ukiyatimiza
hayo utakuwa umenifurahisha sana."
Alinipiga piga mgongoni nikahisi kama nimeshikwa na nyaya za umeme.
Nilitetemeshwa.
Nilimuuliza babu nikiwa na tabasamu "babu sasa kwanini mkuu wenu ameamua
kunichagua mimi ikiwa bado mimi ni binti mdogo? Na nisiye na uwezo wowote
kifedha?"
"swali zuri sana. wakati wote nakueleza kuwa mkuu wetu amependezwa na nyota
yako hiyo ndio sababu iliyomvutia mkuu wetu" aliyameza mate kisha
aliniambia "mkuu wetu ana utajiri mkubwa yeye haihitaji sadaka" kisha babu
alicheka kifedhuli.
niliacha kuuliza maswali na kuendelea kuzuru Gamboshi kama mtalii. Nikaona
kikao kimoja klichohudhuriwa na watu wengi sana, kikiwa kinaongozwa na joka
kubwa yaani joka lile lilikuwa kubwa kupitiliza. Joka lile lilikuwa
likiwatemea wale watu mate yake. Cha ajabu mate yake yalikuwa mengi kila
alipokuwa akiwatemea ikawa kama ilikuwa inanyesha mvua. hivyo kila mmoja
aliye katika kikao kile alilowa chapachapa. babu alinieleza kuhusu joka
lile.
"yule ni mdogo sana kwangu, ni mtu wa heshima sana huko Nigeria yeye
hugawa nguvu na kukubalika pamoja na kufunguka kwa milango yao ya pesa
lakini bado hajafika katika wadhifa wangu yeye hapa ni sawa na waziri mkuu
huko duniani" Nilijiuliza sana moyoni
'sasa babu atakuwa ni nani ikiwa huyu nyoka mkubwa, anayetisha angekuwa yu
chini ya babu?' ilibidi nimuulize "sasa wewe ni nani katika wadhifa wako?"
Babu alicheka, wala hakuniambia wadhifa wake. Ila nilimuuliza tena "kwa
hiyo babu wale ni matajiri wa wapi?" alinijibu kwa majivuni "wale ni
matajiri kutoka katika kila pembe ya dunia si wa Nigeria peke yake"
hapo nikawa nimeelewa. Nilimuuliza swali lingine tofauti "hivi babu! yule
mwanamke aliyekuja pale nyumbani siku ya msiba wa mama, akajitambulisha
kuwa alitokea Gamboshi alikuwa ni nani?" hili nalo hakunijibu. Aliita jina
moja nisilolifahamu kwa sauti iliyotetema kama radi. "Consolathaa!" Fumba
na kufumbua mbele yetu akatokea yule mwanamke aliyekuja siku ile nyumbani
kwenye msiba wa mama. Alikuwa ni mchafu na kunuka sana. Alikuwa ni huyo
aliyeitwa na babu kwa jina hilo la Consolatha. Babu akanieleza hadithi fupi
iliyomuhusu Consolatha. "huyu ni mwanangu wa kike wa pekee niliyemzaa
baada ya baba yako kuacha ziwa katika miaka mitatu iliyopita kwenye uzao wa
bibi yako. Mizimu ikapendezwa naye lakini alifanya kosa dogo la kijinga
katika masharti aliyopewa na mkuu"
wakati ambao babu alikuwa akinielezea hayo, Consolatha alikuwa amepiga
magoti akiwa ameinamisha kichwa chini kwa heshima kama akisujudu mbele yetu.
Babu aliendelea kunieleza "yeye aliambiwa ile damu iwatokayo kila mwezi
ahiifadhi katika kikombe na kukiweka kwenye kitanda alaliacho na baada ya
kukata, amletee mkuu wetu na iwe kama kiapo chake kwa kuinywa kikombe
kimoja" babu alikohoa, akameza mate kisha aliendelea
"yeye alishindwa kwa kuona eti ulikuwa ni uchafu" mimi mwenyewe nilikunja
sura kwa kuona ni uchafu niliona kuwa ni jambo ambalo lisingewezekana.
Kunywa uchafu uliotoka mwilini mwangu? Ni heri niukose huo umalkia.
Nilimsalimia shangazi. Baada ya kuniitikia salamu yangu alitoweka. Babu
akaniambia "hata wewe usithubutu kwenda kinyume na masharti ya mkuu.
Utapata shida huku Gamboshi, duniani na popote utakapokuwa unaenda"
niliteteeka kwa uoga sana. Niliitikia tu bila kumaanisha kama nimeelewa
alichoniambia. Akaniambia tena "sasa muda wa kwenda kukuapisha na kukupa
nguvu umefika. Lakini kama haupo tayari kupewa masharti utakayopewa ni heri
usikubali."
hapo ni kawa mzito kukubali. Sikujua niseme lipi kati ya "ndiyo ama hapana"
lakini nilijipa moyo kuwa masharti ambayo ningepewa huenda ningeyaweza. Babu
akaniamuru nivue nguo nilizovaa "vua zote ubaki kama ulivyozaliwa"
Nilikataa.
"usiogope, hutabaki uchi kila mahali utakapokuwa unaenda, kuna nguo ambazo
nitakuvalisha kwa ajili ya utukufu mbele za mkuu" Bado nilikataa. Punde si
punde dakika chache mbele nilijishangaa kuona nimevaa gauni lenye rangi ya
zambarau. Kiunoni mshipi wa rangi ya damu ya mzee pamoja na viatu vya rangi
ya dhahabu. Hakika nilipendeza sana. Nilipendeza kupitiliza. Nywele zangu
zikawa laini kama sufi na ngozi yangu iliteleza kama mtoto mdogo. Ule uzuri
niliokuwa nikisifiwa kule duniani, niliona kama uchafu, huku Gamboshi
ulikuwa maradufu. Nilitamani kujitazama muda wote. Tabasamu likanipoyoka
na kumzawadia babu lile maridhawa. Babu alikuwa akinitazama huku
akitabasamu kiukweli.
aliniambia. "nilikueleza huku hakuna kinachoshindikana" kisha tulipotea na
kutokezea katikati ya kundi kubwa la watu. Wake kwa waume wakiwa wamefurahi
kupita kiasi.
Nilimuuliza babu "Hawa wamefurahi nini?"
Babu alikuwa na furaha sana siku hiyo, alinishika mabegani na kuniambia
"hawa wote wapo eneo hili kushuhudia msichana wa kwanza akikabidhiwa
mamlaka makubwa na mazito ndani ya Gamboshi haijapata kuwahi kutokea tangu
kuumbwa kwa ulimwengu msichana aliyechaguliwa na mkuu mwenyewe wa ulimwengu
huu. hakika ni furaha iliyoje kwa ukoo wangu na watu wote wa Matonde" babu
alicheka sana. Alicheka, akacheka kupitiliza. mimi nilijisikia ufahari
kuona kila mtu akicheza na kunisujudia mbele yangu. Watu walikuwa ni wengi
sana. Wengi walikuwa wamefunika sehemu zao za siri na ngozi ya mnyama. Fisi
na wanyama wengine nao walikuwepo kila nyuso iliyokuwa mahali pale
ilionesha uchangamfu na furaha iliyoje nilicheka usoni na moyoni tabasamu
likachanua hakika. kikaja kiumbe cha ajabu. Kiumbe kilichotetemesha
Gamboshi nzima.
hugawa nguvu na kukubalika pamoja na kufunguka kwa milango yao ya pesa
lakini bado hajafika katika wadhifa wangu yeye hapa ni sawa na waziri mkuu
huko duniani" Nilijiuliza sana moyoni
'sasa babu atakuwa ni nani ikiwa huyu nyoka mkubwa, anayetisha angekuwa yu
chini ya babu?' ilibidi nimuulize "sasa wewe ni nani katika wadhifa wako?"
Babu alicheka, wala hakuniambia wadhifa wake. Ila nilimuuliza tena "kwa
hiyo babu wale ni matajiri wa wapi?" alinijibu kwa majivuni "wale ni
matajiri kutoka katika kila pembe ya dunia si wa Nigeria peke yake"
hapo nikawa nimeelewa. Nilimuuliza swali lingine tofauti "hivi babu! yule
mwanamke aliyekuja pale nyumbani siku ya msiba wa mama, akajitambulisha
kuwa alitokea Gamboshi alikuwa ni nani?" hili nalo hakunijibu. Aliita jina
moja nisilolifahamu kwa sauti iliyotetema kama radi. "Consolathaa!" Fumba
na kufumbua mbele yetu akatokea yule mwanamke aliyekuja siku ile nyumbani
kwenye msiba wa mama. Alikuwa ni mchafu na kunuka sana. Alikuwa ni huyo
aliyeitwa na babu kwa jina hilo la Consolatha. Babu akanieleza hadithi fupi
iliyomuhusu Consolatha. "huyu ni mwanangu wa kike wa pekee niliyemzaa
baada ya baba yako kuacha ziwa katika miaka mitatu iliyopita kwenye uzao wa
bibi yako. Mizimu ikapendezwa naye lakini alifanya kosa dogo la kijinga
katika masharti aliyopewa na mkuu"
wakati ambao babu alikuwa akinielezea hayo, Consolatha alikuwa amepiga
magoti akiwa ameinamisha kichwa chini kwa heshima kama akisujudu mbele yetu.
Babu aliendelea kunieleza "yeye aliambiwa ile damu iwatokayo kila mwezi
ahiifadhi katika kikombe na kukiweka kwenye kitanda alaliacho na baada ya
kukata, amletee mkuu wetu na iwe kama kiapo chake kwa kuinywa kikombe
kimoja" babu alikohoa, akameza mate kisha aliendelea
"yeye alishindwa kwa kuona eti ulikuwa ni uchafu" mimi mwenyewe nilikunja
sura kwa kuona ni uchafu niliona kuwa ni jambo ambalo lisingewezekana.
Kunywa uchafu uliotoka mwilini mwangu? Ni heri niukose huo umalkia.
Nilimsalimia shangazi. Baada ya kuniitikia salamu yangu alitoweka. Babu
akaniambia "hata wewe usithubutu kwenda kinyume na masharti ya mkuu.
Utapata shida huku Gamboshi, duniani na popote utakapokuwa unaenda"
niliteteeka kwa uoga sana. Niliitikia tu bila kumaanisha kama nimeelewa
alichoniambia. Akaniambia tena "sasa muda wa kwenda kukuapisha na kukupa
nguvu umefika. Lakini kama haupo tayari kupewa masharti utakayopewa ni heri
usikubali."
hapo ni kawa mzito kukubali. Sikujua niseme lipi kati ya "ndiyo ama hapana"
lakini nilijipa moyo kuwa masharti ambayo ningepewa huenda ningeyaweza. Babu
akaniamuru nivue nguo nilizovaa "vua zote ubaki kama ulivyozaliwa"
Nilikataa.
"usiogope, hutabaki uchi kila mahali utakapokuwa unaenda, kuna nguo ambazo
nitakuvalisha kwa ajili ya utukufu mbele za mkuu" Bado nilikataa. Punde si
punde dakika chache mbele nilijishangaa kuona nimevaa gauni lenye rangi ya
zambarau. Kiunoni mshipi wa rangi ya damu ya mzee pamoja na viatu vya rangi
ya dhahabu. Hakika nilipendeza sana. Nilipendeza kupitiliza. Nywele zangu
zikawa laini kama sufi na ngozi yangu iliteleza kama mtoto mdogo. Ule uzuri
niliokuwa nikisifiwa kule duniani, niliona kama uchafu, huku Gamboshi
ulikuwa maradufu. Nilitamani kujitazama muda wote. Tabasamu likanipoyoka
na kumzawadia babu lile maridhawa. Babu alikuwa akinitazama huku
akitabasamu kiukweli.
aliniambia. "nilikueleza huku hakuna kinachoshindikana" kisha tulipotea na
kutokezea katikati ya kundi kubwa la watu. Wake kwa waume wakiwa wamefurahi
kupita kiasi.
Nilimuuliza babu "Hawa wamefurahi nini?"
Babu alikuwa na furaha sana siku hiyo, alinishika mabegani na kuniambia
"hawa wote wapo eneo hili kushuhudia msichana wa kwanza akikabidhiwa
mamlaka makubwa na mazito ndani ya Gamboshi haijapata kuwahi kutokea tangu
kuumbwa kwa ulimwengu msichana aliyechaguliwa na mkuu mwenyewe wa ulimwengu
huu. hakika ni furaha iliyoje kwa ukoo wangu na watu wote wa Matonde" babu
alicheka sana. Alicheka, akacheka kupitiliza. mimi nilijisikia ufahari
kuona kila mtu akicheza na kunisujudia mbele yangu. Watu walikuwa ni wengi
sana. Wengi walikuwa wamefunika sehemu zao za siri na ngozi ya mnyama. Fisi
na wanyama wengine nao walikuwepo kila nyuso iliyokuwa mahali pale
ilionesha uchangamfu na furaha iliyoje nilicheka usoni na moyoni tabasamu
likachanua hakika. kikaja kiumbe cha ajabu. Kiumbe kilichotetemesha
Gamboshi nzima.
ulikuja upepo ukavuma kwa muda mrefu sana. Kabla ya kusikika kelele za hapa
na pale, kulikuwa na radi iliyopiga na kutoa cheche kutoka kila kona ya
sehemu zote za Gamboshi. Ufinyu wa mwanga haukuwepo tena, kiumbe hicho
kiling'aa sana. Kilikuwa ni kiumbe kirefu na kikubwa sana. Kila kiumbe
hapo Gamboshi kilisujudu mbele ya kiumbe kile, hata babu pia. Mimi
sikufanya chochote kwakuwa nilikuwa nimekalishwa mbele ya kiti pembeni na
ambacho angekaa yeye kiumbe huyo. Alikuwa na macho yaliyong'aa sana. Mfano
wa macho yake yalivyong'aa ni sawa na paka uliyemmulika gizani sehemu za
machoni. Hakuwa na macho mawili, jicho moja tu tena lilining'inia juu ya
paji la uso. Mdomo wake ulikuwa mkubwa sana na kichwa chake kilikuwa kama
ndege aina ya korongo. Wote waliosujudu waliongea vitu ambavyo haikuwa
rahisi mimi kufahamu walizungumza nini. Lakini waliongea lugha ya tofauti
na Kiswahili na wala haikuwa kiingereza. Niliendelea kuwatazama, wakati
kiumbe yule wa ajabu mwenye mwili wa nyoka sehemu ya chini ya kiuno chake
baada ya kiwiliwili cha juu , kukaa sehemu aliyoandaliwa. Yeye alivaa joho
la rangi ya dhahabu. Dhahabu iliyong'aa sana. Hata viatu vyake vilikuwa ni
dhahabu tupu. Alikuwa anatoa ala za muziki kila atembeapo. Ala zile
zilipendeza sana kuzisikiliza. Kichwani alikuwa na taji la dhahabu
lililomeremeta sana. Alishika kitabu Fulani kikubwa ambacho sikukifahamu.
Alionesha kuwa na furaha sana. Alipokuwa akinitazama muda wote, alikuwa
akicheka kwa furaha.
aliliita jina langu huku akicheka
"Bella"
kabla sijageuka kukitazama kile kiumbe, eneo lote la Gamboshi likalipuka
kwa makofi yaliyokuwa yakipigwa kila kona ya mkutano huo. Niliogopa sana
kukaa karibu na kile kiumbe. Kikiongea kilikuwa kinatema moto
nikamfananisha na zile katuni za dragoni. Mwili wote ulijaa jasho kwa uoga.
Kile kiumbe kilitamka
"usiogope mwanangu Bella"
kikacheka sana, kisha kiumbe kile kikaendelea kuniambia
"mimi ni mkuu wa wakuu wa ulimwengu huu. Mimi ndiye baba wa wababa wa
vizazi vyako vyote vilivyopita. Mimi ndiye niliyekuandaa wewe kuja kurithi
falme atakayoiacha Babu yako Mzee Matonde, mimi ndiye Lucifer mtakatifu
kuliko wote awaye"
nilshituka kwa mshangao ambao sikutarajia. Sikuzimia kutokana na hali kuwa
mbaya eneo hilo. Macho yangu yalipokuwa yakielekea eneo la usingizi mzito
wa kupoteza fahamu, mimi nilishindwa kuzimia kutokana na uoga.
Nilimkodolea macho.
Sikuamini ambacho kilikuwa kikitokea kwa wakati huo, Niliona kama ndoto.
Kiumbe kile kikabadilika kikawa binadamu aliyevutia sana. Alikuwa ni mzuri
kuliko mvulana mzuri yeyote ambaye uliwahi kumuona duniani.
Hakikutisha tena.
kila kiumbe katika mji wa Gamboshi kilipiga kelele. Yule kiumbe wa ajabu
akafura kwa sifa kwa heshima aliyopewa.
Alisema
"ninao utajiri wa kutosha pamoja na nguvu nyingi. Mimi si mchoyo kwa yeyote
aniombaye. Hutoa vipawa na karama kwa kila mtu anifuataye. Mimi humbariki
kila mmoja lakini kuna adhabu kali kwa yeyote akiukaye maagizo yangu"
nilimuona yue mtu aliyejiita Lucifer, akiwa amefura kwa hasira na uso wake
kujikunja sana. Hakika alikuwa na hasira na ghadhabu sana. Mimi sikuwa
nikimsikiliza kwa umakini ila niliogopa sana kwa kuwa sikuamini kama
nimekaa karibu kabisa na yule wanayemuita shetani. Niliwaza mengi sana.
Nilitetemeka kwa uoga lakini haikusaidia.
labda nikuambie kitu. Huyu kiumbe ndiye yule aliyewahi kuwa mmoja wa
malaika wakuu huko mbinguni. Yeye alikuwa na kazi ya kumsifu na kumuimbia
mungu.
Aliitwa Lucifer.
baada ya kujiona yeye ni mmoja kati ya malaika walioumbwa vizuri kuliko
malaika wote, akapatwa na kiburi. Kiburi cha kutaka kumpindua mungu. Kama
utakumbuka mwanzo wa safari yangu ya huku Gamboshi, nilimuuliza babu kuhusu
ule mji ambao niliuona kwa mbali ukiwa unang'aa na kupendeza. Akaniambia
kuwa ule si mji mzuri kufikiria wala kutamani kuingia. Akasema kuwa kule
ndipo alipokuwepo mkuu wao hapo mwanzo. Basi eneo lile naweza kusema ndio
mbinguni na yeye Lucifer akatupwa ulimwenguni katika ziwa la moto. Kutokana
na adhabu kuwa kali, aliapa kuondoka na kila mwanadamu wa kumdanganya. Ila
kipindi hiki ambacho nilikuwa Gamboshi sikuweza kuwa na ufahamu wa kutosha.
Hivyo niliendelea kukaa nikifurahia utukufu niliopewa. Watu walianguka
miguuni mwangu kwa kusujudu. Nilijisikia ufahari sana. Sikujuwa kuwa
nilifungwa ufahamu wangu.
yule kiumbe wa ajabu akaendelea.
"leo nitakukabidhi utawala wa babu yako. Utawala wa kusimamia Gamboshi na
kushika wadhifa mkubwa Duniani. Utakuwa mtu wa heshima hapa na huko
duniani. Utajiri utakutafuta na si kuutafuta kwa jasho. Mdomo wako utakuwa
Baraka kwa kila ukinenacho na kukitamka. Laana iwe juu ya kila mtu
atakayekulaani"
babu alisogea mbele yangu. Babu alikuwa amevaa joho la rangi ya zambarau
pia, kama gauni langu. Alikuwa amevaa taji kubwa kichwani mwake. Alishika
fimbo mkononi.
yule kiumbe wa ajabu alipomuona babu, alicheka kwa sauti kubwa sana.
hakucheka kwa karaha bali fedheha. Hapa nikagundua mbali ya ubinadamu
halisi hakuna kiume kilichocheka kwa kumaanisha furaha halali. Babu
alilivua taji lake na kunivisha mimi, pamoja na kunikabidhi pete yake.
Fimbo yake pia alinipatia; yule kiumbe wa ajabu akapaza sauti
"nakukabidhi rasmi utawala wa babu yako. Utawala uliotukuka Gamboshi na
ulimwenguni kote. Upate heshima nchini mwako na nje ya nchi. Uwe na utajiri
wa kutosha kwa kutumia pete hiyo. Fimbo hiyo itibu kila ugonjwa
utakaosumbua kila mtu akuombaye msaada, taji hilo uwe malkia wa ulimwengu
mzima lakini hayo yote ni baada ya kutimiza masharti haya nikupayo"
alinyamaza kwa muda kabla hajaendelea. Babu alinitazama kwa jicho la
huzuni. Sikujua ilikuwa hivyo kwanini.
na pale, kulikuwa na radi iliyopiga na kutoa cheche kutoka kila kona ya
sehemu zote za Gamboshi. Ufinyu wa mwanga haukuwepo tena, kiumbe hicho
kiling'aa sana. Kilikuwa ni kiumbe kirefu na kikubwa sana. Kila kiumbe
hapo Gamboshi kilisujudu mbele ya kiumbe kile, hata babu pia. Mimi
sikufanya chochote kwakuwa nilikuwa nimekalishwa mbele ya kiti pembeni na
ambacho angekaa yeye kiumbe huyo. Alikuwa na macho yaliyong'aa sana. Mfano
wa macho yake yalivyong'aa ni sawa na paka uliyemmulika gizani sehemu za
machoni. Hakuwa na macho mawili, jicho moja tu tena lilining'inia juu ya
paji la uso. Mdomo wake ulikuwa mkubwa sana na kichwa chake kilikuwa kama
ndege aina ya korongo. Wote waliosujudu waliongea vitu ambavyo haikuwa
rahisi mimi kufahamu walizungumza nini. Lakini waliongea lugha ya tofauti
na Kiswahili na wala haikuwa kiingereza. Niliendelea kuwatazama, wakati
kiumbe yule wa ajabu mwenye mwili wa nyoka sehemu ya chini ya kiuno chake
baada ya kiwiliwili cha juu , kukaa sehemu aliyoandaliwa. Yeye alivaa joho
la rangi ya dhahabu. Dhahabu iliyong'aa sana. Hata viatu vyake vilikuwa ni
dhahabu tupu. Alikuwa anatoa ala za muziki kila atembeapo. Ala zile
zilipendeza sana kuzisikiliza. Kichwani alikuwa na taji la dhahabu
lililomeremeta sana. Alishika kitabu Fulani kikubwa ambacho sikukifahamu.
Alionesha kuwa na furaha sana. Alipokuwa akinitazama muda wote, alikuwa
akicheka kwa furaha.
aliliita jina langu huku akicheka
"Bella"
kabla sijageuka kukitazama kile kiumbe, eneo lote la Gamboshi likalipuka
kwa makofi yaliyokuwa yakipigwa kila kona ya mkutano huo. Niliogopa sana
kukaa karibu na kile kiumbe. Kikiongea kilikuwa kinatema moto
nikamfananisha na zile katuni za dragoni. Mwili wote ulijaa jasho kwa uoga.
Kile kiumbe kilitamka
"usiogope mwanangu Bella"
kikacheka sana, kisha kiumbe kile kikaendelea kuniambia
"mimi ni mkuu wa wakuu wa ulimwengu huu. Mimi ndiye baba wa wababa wa
vizazi vyako vyote vilivyopita. Mimi ndiye niliyekuandaa wewe kuja kurithi
falme atakayoiacha Babu yako Mzee Matonde, mimi ndiye Lucifer mtakatifu
kuliko wote awaye"
nilshituka kwa mshangao ambao sikutarajia. Sikuzimia kutokana na hali kuwa
mbaya eneo hilo. Macho yangu yalipokuwa yakielekea eneo la usingizi mzito
wa kupoteza fahamu, mimi nilishindwa kuzimia kutokana na uoga.
Nilimkodolea macho.
Sikuamini ambacho kilikuwa kikitokea kwa wakati huo, Niliona kama ndoto.
Kiumbe kile kikabadilika kikawa binadamu aliyevutia sana. Alikuwa ni mzuri
kuliko mvulana mzuri yeyote ambaye uliwahi kumuona duniani.
Hakikutisha tena.
kila kiumbe katika mji wa Gamboshi kilipiga kelele. Yule kiumbe wa ajabu
akafura kwa sifa kwa heshima aliyopewa.
Alisema
"ninao utajiri wa kutosha pamoja na nguvu nyingi. Mimi si mchoyo kwa yeyote
aniombaye. Hutoa vipawa na karama kwa kila mtu anifuataye. Mimi humbariki
kila mmoja lakini kuna adhabu kali kwa yeyote akiukaye maagizo yangu"
nilimuona yue mtu aliyejiita Lucifer, akiwa amefura kwa hasira na uso wake
kujikunja sana. Hakika alikuwa na hasira na ghadhabu sana. Mimi sikuwa
nikimsikiliza kwa umakini ila niliogopa sana kwa kuwa sikuamini kama
nimekaa karibu kabisa na yule wanayemuita shetani. Niliwaza mengi sana.
Nilitetemeka kwa uoga lakini haikusaidia.
labda nikuambie kitu. Huyu kiumbe ndiye yule aliyewahi kuwa mmoja wa
malaika wakuu huko mbinguni. Yeye alikuwa na kazi ya kumsifu na kumuimbia
mungu.
Aliitwa Lucifer.
baada ya kujiona yeye ni mmoja kati ya malaika walioumbwa vizuri kuliko
malaika wote, akapatwa na kiburi. Kiburi cha kutaka kumpindua mungu. Kama
utakumbuka mwanzo wa safari yangu ya huku Gamboshi, nilimuuliza babu kuhusu
ule mji ambao niliuona kwa mbali ukiwa unang'aa na kupendeza. Akaniambia
kuwa ule si mji mzuri kufikiria wala kutamani kuingia. Akasema kuwa kule
ndipo alipokuwepo mkuu wao hapo mwanzo. Basi eneo lile naweza kusema ndio
mbinguni na yeye Lucifer akatupwa ulimwenguni katika ziwa la moto. Kutokana
na adhabu kuwa kali, aliapa kuondoka na kila mwanadamu wa kumdanganya. Ila
kipindi hiki ambacho nilikuwa Gamboshi sikuweza kuwa na ufahamu wa kutosha.
Hivyo niliendelea kukaa nikifurahia utukufu niliopewa. Watu walianguka
miguuni mwangu kwa kusujudu. Nilijisikia ufahari sana. Sikujuwa kuwa
nilifungwa ufahamu wangu.
yule kiumbe wa ajabu akaendelea.
"leo nitakukabidhi utawala wa babu yako. Utawala wa kusimamia Gamboshi na
kushika wadhifa mkubwa Duniani. Utakuwa mtu wa heshima hapa na huko
duniani. Utajiri utakutafuta na si kuutafuta kwa jasho. Mdomo wako utakuwa
Baraka kwa kila ukinenacho na kukitamka. Laana iwe juu ya kila mtu
atakayekulaani"
babu alisogea mbele yangu. Babu alikuwa amevaa joho la rangi ya zambarau
pia, kama gauni langu. Alikuwa amevaa taji kubwa kichwani mwake. Alishika
fimbo mkononi.
yule kiumbe wa ajabu alipomuona babu, alicheka kwa sauti kubwa sana.
hakucheka kwa karaha bali fedheha. Hapa nikagundua mbali ya ubinadamu
halisi hakuna kiume kilichocheka kwa kumaanisha furaha halali. Babu
alilivua taji lake na kunivisha mimi, pamoja na kunikabidhi pete yake.
Fimbo yake pia alinipatia; yule kiumbe wa ajabu akapaza sauti
"nakukabidhi rasmi utawala wa babu yako. Utawala uliotukuka Gamboshi na
ulimwenguni kote. Upate heshima nchini mwako na nje ya nchi. Uwe na utajiri
wa kutosha kwa kutumia pete hiyo. Fimbo hiyo itibu kila ugonjwa
utakaosumbua kila mtu akuombaye msaada, taji hilo uwe malkia wa ulimwengu
mzima lakini hayo yote ni baada ya kutimiza masharti haya nikupayo"
alinyamaza kwa muda kabla hajaendelea. Babu alinitazama kwa jicho la
huzuni. Sikujua ilikuwa hivyo kwanini.
ITAENDELEA!!!
No comments:
Post a Comment